Shahada
-
Tarehe 25 Shawwal Mwaka 148 Hijiria, ulimwengu wa Kiislamu ulipatwa na Huzuni kufuatia kuondokewa na mmoja wa Ahlul-Bayti wa Mtume wa Uislamu (saww)
Licha ya kwamba Ahlul-Bayti wa Mtume (s.a.w.w) walikabiliwa na changamoto tofauti kisiasa na kijamii, lakini walijitahidi kuhakikisha wanainua bendera ya dini ya Kiislamu katika zama zao zote. Dakta Shahid Mutwahhari, mwanafikra mashuhuri wa Iran anaandika kwa kusema: " Ahlul-Bayti (a.s) walikuwa wakichunga maslahi ya Kiislamu na Waislamu kwa ujumla".
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.
-
Wasifu wa Amirul Momineen (AS) unapaswa kuunganisha mwili wa Umma wa Kiislamu
Katika hotuba yake kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Imam Ali, Waziri Mkuu wa Iraq alitaja fadhila za Imam Ali (a.s).
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".
-
Sehemu ya Fadhila za Kipekee za Imam Ali (a.s):
Imam Ali (a.s) ni Mtu wa Kwanza kuzaliwa ndani ya Msikiti na Kuuliwa ndani ya Msikiti
Imam Ali (a.s), Maisha yake yote yalikuwa ni Maisha ya kuweka uthabiti na kuimarisha nguzo na misingi ya Uislamu, pia kujitolea muhanga kwa kitu ghali na chenye thamani kubwa, ili kuhakikisha neno la Mwenyezi Mungu linakuwa juu, na neno la makafiri linakuwa chini.