Shahada
-
Upendo na Uaminifu Usio na Kikomo kwa Muqawama na Wilayat; Kumbukumbu ya Mashahidi Nasrallah na Safiyyu al-Din
Katika kumbukumbu ya mwaka wa kwanza wa mazishi ya mashahidi wa Hezbollah, Hassan Nasrallah na Hashim Safiyyu al-Din, Naim Qassem alisisitiza kuendelea kwa njia ya Muqawama na uaminifu (Wilayat) kwa Kiongozi Sayyid Ali Khamenei, akieleza kuwa Muqawama hauwezi kushindwa iwe kwa ushindi au kwa shahada.
-
Majlis ya Kuhuisha Shahada ya Sayyidat Fatima Al-Zahra (sa) kwa Akina Mama Jijini Dar es Salaam +Picha
Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.
-
Hizbullah Yatangaza Kuuawa Shahidi kwa Kamanda Wake Mwandamizi, Abu Ali Tabatabai
Hizbullah ya Lebanon imetangaza kwamba mmoja wa makamanda wake mashuhuri, Haitham Tabatabai (Abu Ali), ameuliwa shahidi katika shambulio la anga lililofanywa leo na Israel.
-
Mahakama Kuu Yaweza Kuongeza Ufanisi wa Mfumo wa Kiislamu Kupitia Utekelezaji wa Haki
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s), akiwa mbele ya wakurugenzi na wafanyakazi wa Mahakama ya Mkoa wa Gilan, amesema kuwa utekelezaji sahihi wa haki na usawa katika taasisi zote za serikali unaweza kuongeza ufanisi wa Jamhuri ya Kiislamu na kuthibitisha madai yake ya msingi kuhusu haki katika utawala.
-
Mazishi ya Mashahidi 300 Wasiojulikana Kufanyika Siku ya Kumbukumbu ya Shahada ya Bi.Fatima(sa); Dalili ya Umoja wa Kitaifa Baada ya Vita vya Siku 12
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (IRGC) wa Mkoa Mkuu wa Tehran, Sardar Hassanzadeh, amesema kuwa miili ya mashahidi 300 wasiojulikana—ikiwa ni pamoja na 200 kwa mikoa mbalimbali na 100 kwa jiji la Tehran—iko tayari kwa ajili ya mazishi ya kitaifa. Mazishi haya yatafanyika Jumatatu tarehe 3 Azar, sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a.s), ambapo msafara maalumu wa “Lale za Fatima” utaanza saa 2:00 asubuhi mbele ya Chuo Kikuu cha Tehran kuelekea kwenye kituo cha "Meraje’ Shohada".
-
Maadhimisho ya Mwaka wa kwanza wa Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah yatafanyika Siku ya Alhamisi
Baraza la Kuratibu Tablighi la Kiislamu limetangaza katika taarifa yake kwamba maadhimisho ya mwaka wa kwanza wa kifo cha shahidi Sayyid Hassan Nasrallah yatafanyika Alhamisi, tarehe 02 Oktoba, 2025, katika nchi nzima, chini ya kauli mbiu kuu “Innā ‘ala al-‘Ahd”. Hafla kuu itafanyika saa 4:00 usiku katika Uwanja wa Ibada wa Imam Hussein (a.s) mjini Teheran.
-
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan: Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah Imeongeza Msaada wa Kijamii kwa Hizbullah
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan, kwa mnasaba wa kumbukumbu ya mwaka wa kwanza wa shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, alisema: Shahidi Hassan Nasrallah alikuwa mjahid mkubwa katika zama zake, na kwa shahada yake msaada na uungaji mkono wa kijamii kwa Hizbullah umeongezeka.
-
Mkutano wa Wanafunzi wanaoongea Lugha ya Kiurdu Wanaokaa Mjini Qom - Iran; katika Kumbukumbu ya Mwaka wa Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah
Hujjatul-Islam Fakhrian aliandika mada yake kwa kuanzia na nukuu ya Kiungu (alirejea aya za Quran) na kutangaza kuwa: azma ya Mwenyezi Mungu ni kuwapa walio dhaifu nafasi ya kuwa waanzilishi na warithi wa dunia; azma hiyo inatimia kwa njia moja tu — kupitia mapambano na kujitolea. Kwa hivyo, alisisitiza, hakuna njia nyingine ya kuangusha mfumo wa udikteta wa kigeni isipokuwa kupitia mapambano.
-
Shahidi Sayed Hasan Nasrallah kwa maneno ya binti yake wa pekee
Kituo cha habari “Asr” kimechapisha mahojiano ya kwanza ya kipekee na Zainab Nasrallah, binti wa pekee wa shahidi Sayed Hasan Nasrallah.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu:
"Ushahidi (shahada) ni thawabu ya jitihada za jihadi; iwe katika utetezi wa miaka 8, au katika mapambano ya kishujaa ya siku 12"
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika ujumbe wake kwa mnasaba wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu, aliitaja shahada kuwa ni thawabu ya juhudi za jihadi, na alisisitiza juu ya umuhimu wa kujitolea huku katika kukuza mataifa. Vilevile, alieleza yakini yake juu ya ushindi wa haki na umuhimu wa kushikamana na majukumu ya kidini.
-
Katika mazungumzo na ABNA:
Ushuhuda wa Dada wa Shahidi Abbas Mousavi Kuhusu Kiongozi wa Muqawama:Syed alikuwa Mpenzi wa Mungu -Tulipata nguvu na matumaini kutoka kwa hotuba zake
Bi Hoda Mousavi, dada wa shahidi Sayed Abbas Mousavi, Katibu Mkuu wa zamani wa Hezbollah Lebanon, amesema: Sisi daima tulihisi katika maneno na mwongozo wake kwamba yeye kwanza kabisa alikuwa mpenzi wa Mungu. Mara tu tuliposikiliza hotuba zake, tulivutiwa kimagnet kwa hisia kwake; siri ya hilo ilikuwa katika ikhlasi na uaminifu wake kwa mpenzi wake wa kimungu.
-
Majlisi ya Kumbukumbu ya Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah Kufanyika Beirut
Katika hafla hiyo: Mzungumzaji mkuu atakuwa Sheikh Muhammad Sadiq.
-
Ustahimilivu wa waandishi wa habari wa Yemen kutoka Sana'a hadi Gaza:
Kuanzia kwa kuuawa shahidi kwa waandishi wa habari 32 wa Kiyemeni hadi kusimama imara kwa mwandishi wa Al-Masirah chini ya mashambulizi ya mabomu Gaza
Waandishi wa habari wa Kiyemeni walipaa (walipata shahada) wakiwa wamesimama imara katika 'uwanja wa maneno', wakikabiliana na adui na 'mradi wa uharibifu wa uvamizi wa kimataifa' unaoongozwa na Marekani, hadi wakapata shahada.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu:
“Haiwezekani kuupiga magoti Umma wa Iran na Mfumo wa Kiislamu kupitia vita"
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, katika maadhimisho ya kumbukumbu ya Shahada ya Imam Ridha (a.s), amesema: "Umma wa Iran na Mfumo wa Kiislamu hauwezi kupigwa magoti kwa vita na kulazimishwa kusalimu amri"
-
Imam Baqir (a.s): Kutoka Machozi hadi Fikra
"Ninapokusoma jina lako, nakushukuru kwa ukubwa wa maarifa yako, na pia nakumbuka machozi yako ya utotoni huko Karbala...". Maisha ya Imam Muhammad Baqir (a.s) yamejazwa na mafundisho ya kina na nyakati za tafakari ambazo hazileti tu machozi kwa mioyo bali pia huamsha fikra na akili. Katika kipindi kigumu cha historia, alitumia hekima na maarifa kuleta mwanga mpya katika mafahimu za Dini.
-
Tarehe 25 Shawwal Mwaka 148 Hijiria, ulimwengu wa Kiislamu ulipatwa na Huzuni kufuatia kuondokewa na mmoja wa Ahlul-Bayti wa Mtume wa Uislamu (saww)
Licha ya kwamba Ahlul-Bayti wa Mtume (s.a.w.w) walikabiliwa na changamoto tofauti kisiasa na kijamii, lakini walijitahidi kuhakikisha wanainua bendera ya dini ya Kiislamu katika zama zao zote. Dakta Shahid Mutwahhari, mwanafikra mashuhuri wa Iran anaandika kwa kusema: " Ahlul-Bayti (a.s) walikuwa wakichunga maslahi ya Kiislamu na Waislamu kwa ujumla".
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.
-
Wasifu wa Amirul Momineen (AS) unapaswa kuunganisha mwili wa Umma wa Kiislamu
Katika hotuba yake kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Imam Ali, Waziri Mkuu wa Iraq alitaja fadhila za Imam Ali (a.s).
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".
-
Sehemu ya Fadhila za Kipekee za Imam Ali (a.s):
Imam Ali (a.s) ni Mtu wa Kwanza kuzaliwa ndani ya Msikiti na Kuuliwa ndani ya Msikiti
Imam Ali (a.s), Maisha yake yote yalikuwa ni Maisha ya kuweka uthabiti na kuimarisha nguzo na misingi ya Uislamu, pia kujitolea muhanga kwa kitu ghali na chenye thamani kubwa, ili kuhakikisha neno la Mwenyezi Mungu linakuwa juu, na neno la makafiri linakuwa chini.