pakistan
-
Himaya thabiti ya Allama Sajid Naqvi kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi/Syed Khamenei Shkhsia wa Kimataifa anayeheshimika katika Ulimwengu wa Kiislamu
Akikosoa matamshi ya hivi karibuni ya kimatusi dhidi ya Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni Shakhsia mwenye hadhi ya Kimataifa katika Umma wa Kiislamu, na kauli yoyote ya kumtusi inaweza kuwa na matokeo mabaya na ya kutia wasiwasi.
-
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan: Iran Imeshinda Vita
"Nachukua fursa hii kuipongeza Serikali na watu wa Iran kwa ushindi huu".
-
Mwanazuoni wa Kishia wa Pakistani:
Uungaji mkono wa Serikali ya Pakistan kwa Iran ni hatua ya kijasiri na ya kupongezwa
Katibu Mkuu wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amepongeza uungaji mkono wa serikali ya Pakistan kwa Iran dhidi ya mashambulizi ya Israel na ameitaja hatua hiyo kuwa ya kijasiri na ya kupongezwa na kuzitaka nchi za Kiislamu kuchukua misimamo thabiti dhidi ya uvamizi wa Wazayuni.
-
Kiongozi wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Watu wa Gilgit-Baltistan hawatakaa kimya mbele ya dhulma; hata wakikata shingo zetu au kukata ndimi zetu, hatutawahi kumuunga mkono dhalimu
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan alisisitiza kuwa kusimama dhidi ya dhulma ni jambo lililo katika damu ya watu wa Gilgit-Baltistan, na hakuna nguvu yoyote inayoweza kunyamazisha sauti yao ya kudai haki.
-
Ayatollah Khamenei: Umoja wa Mataifa ya Kiislamu Ndiyo Njia Pekee ya Kudumisha Usalama wa Umma
Msimamo wa Pakistan kuhusu suala la Palestina umekuwa wa kupongezwa sana. Wakati daima kumekuwa na vishawishi kwa nchi za Kiislamu kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni, Pakistan haijawahi kushawishika na vishawishi hivyo.
-
Iran na Pakistan Zaahidi Ushirikiano wa Kiuchumi na Usalama
Mazungumzo ya Iran na Pakistan yanaonesha dhamira ya pamoja ya Iran na Pakistan kuimarisha ushirikiano wa kimkakati, kiuchumi na kiusalama katika kanda.
-
Balozi wa Taliban nchini Qatar: Emirate ya Kiislamu ni ukweli wa Afghanistan / Iran na India hawaiweki Taliban tena chini ya ushawishi wa Pakistan
Suhail Shahin, balozi wa Taliban nchini Qatar, katika mazungumzo na kituo cha Al Jazeera amesema kwamba Iran na India walidhani Taliban ni tegemezi wa Pakistan, lakini sasa wamegundua kuwa fikra hiyo si ya kweli.
-
India na Pakistan Wakubaliana Kuwarudisha Wanajeshi katika Mipaka ya Awali Kabla ya Mvutano wa Kijeshi
New Delhi na Islamabad Wakubaliana Kuwarejesha Wanajeshi wao katika Nafasi za Kabla ya Mapigano. India na Pakistan wamefikia makubaliano ya kijeshi ya kurejesha vikosi vyao katika mojawapo ya maeneo ya mpaka yaliyokuwa na mvutano, hali ambayo ilizidi kuwa mbaya baada ya shambulio la kigaidi la tarehe 22 Aprili huko Kashmir. Makubaliano haya yamefikiwa baada ya kuongezeka kwa mivutano na mashambulizi ya kuvukiana mipaka, na yanakusudia kupunguza hali ya hatari ya kijeshi kati ya nchi hizo mbili. Kwa mujibu wa taarifa rasmi, urejeshaji wa wanajeshi kwenye nafasi za awali unatarajiwa kukamilika kufikia mwisho wa mwezi Mei.
-
Hatima Isiyojulikana ya Imam wa Ijumaa wa Quetta Nchini Saudi Arabia
Wakati siku 28 zimepita tangu kukamatwa na kupotea kwa Hujjat al-Islam Ghulam Hasnain Wijdani, mchungaji maarufu kutoka Pakistan nchini Saudi Arabia, bado hakuna taarifa yoyote kuhusu hali yake na mahali anaposhikiliwa.
-
Kufanyika kwa Tamasha la Ushairi wa Amani katika mji wa Parachinar, Pakistan / Mkutano wa washairi wa Kishia na Kisunni wenye ujumbe wa umoja
Washairi Mashuhuri wa Kishia na Kisunni kutoka maeneo yote ya Kurram wamekusanyika katika tamasha lenye mada ya amani lililofanyika katika mji wa Parachinar, Pakistan.
-
Watu 5 Wauawa Katika Shambulio la Mizinga la Jeshi la India katika eneo la Kashmir
Watu 5 Wasio Wanajeshi, Wakiwemo Mtoto Mmoja, Wauawa Katika Shambulio la Mizinga la Jeshi la India Katika Eneo la Kashmir Linalodhibitiwa na Pakistan.
-
Onyo Kuhusu Mradi wa "Kuisahau Palestina" – Njama ya Kimataifa kwa Ushirikiano wa Viongozi wa Kiarabu
Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa al-Mustafa: Kusahau Kadhia ya Palestina ni Njama Hatari na Usaliti Usiosameheka. Kiongozi wa Harakati ya Kuamsha Ummah wa Mustafa, katika hotuba yake ya hivi karibuni mjini Lahore, amekosoa vikali ukimya wa ulimwengu wa Kiislamu mbele ya uhalifu wa utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Palestina. Amesema kuwa kusahaulika kwa suala la Palestina ni njama hatari na usaliti usiosameheka, na akasisitiza kwamba ukimya huu – kuanzia vyombo vya habari hadi baadhi ya Serikali za Kiarabu – ni sehemu ya mradi wa kufuta kwa taratibu Palestina kutoka kwenye kumbukumbu ya Ummah wa Kiislamu.
-
Palestina lazima ibaki / Watawala wetu wamepotoka kutoka kwenye Misingi ya Umma wa Kiislamu
Mwenyekiti wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu wa Pakistan akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuiunga mkono Palestina amesema kuwa, watawala na wanasiasa wa sasa wa nchi hiyo wamejitenga na thamani halisi za Umma wa Kiislamu.
-
Maandamano ya “Gaza” Islamabad: Hafidh Naeem atoa wito wa mgomo wa kitaifa na kususia bidhaa za Israel
“Tunaiheshimu nchi yetu, lakini tunataka kuwastua watawala ili wasimame na watu wa Palestina na Kashmir. Ummah wa Kiislamu umelala usingizi wa kutojali.”
-
Mchakato wa kuwatimua wahamiaji wa Afghanistan walioko Pakistan unaanza leo hii
Vyombo vya Habari vya Pakistan vimeripoti kuwa mchakato wa kuwatimua wahamiaji wa Afghanistan bila hati za ukazi wa kisheria kutoka nchi hii umepangwa kuanza leo Jumanne (Aprili 1).
-
Human Rights Watch: Afghanistan si salama kwa wahamiaji waliofukuzwa kutoka Pakistan
Human Rights Watch, katika ripoti yake ya hivi punde kuhusu wahamiaji wa Afghanistan nchini Pakistan, ilionyesha wasiwasi wake kuhusu kufukuzwa kwa lazima kwa wahamiaji hao.
-
Tangazo la Urusi la kuwa tayari kupatanisha Pakistan na Afghanistan
Wakati mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan ukiendelea, Balozi wa Urusi nchini Pakistan alitangaza utayari wa nchi yake kutatua mivutano hii.
-
Radiamali ya Seneta RajA Nasser kwa mauaji ya Mwanazuoni wa Pakistan
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amelaani mauaji ya Mufti Munir Shakir, Mwanazuoni wa Kisunni wa Pakistan, na kuyataja kuwa ni hasara isiyoweza kufidiwa.