Maisha
-
Kutoka Iftari hadi Suhoor: Jinsi Mwezi wa Ramadhani Unavyobadilisha Mzunguko wa Kiuchumi wa Miji
Katika mwezi wa Ramadhani, shughuli za kiuchumi hazibaki tu wakati wa mchana; usiku pia hubadilika kuwa kipindi cha shughuli nyingi za biashara na mwingiliano wa kijamii. Miji hukaa hai usiku kutokana na iftari, usiku wa ibada (Taraweeh), na mikutano ya kijamii, jambo linalochochea biashara za chakula, migahawa, maduka ya bidhaa za kidini, na masoko ya jioni. Aidha, mikutano ya kijamii na iftari za pamoja huimarisha mshikamano wa kijamii, huku pia zikichangia katika mzunguko wa fedha ndani ya jamii. Kwa kifupi, Ramadhani hubadilisha mzunguko wa kiuchumi wa miji kutoka mchana hadi usiku, na kuunda uchumi wa kipekee unaounganisha biashara na maisha ya kijamii.
-
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Woldan:
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kurekebisha mtindo wa maisha
Mkurugenzi Mkuu wa Tablighi za Kiislamu mkoa wa Fars ameeleza kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kujenga upya roho na kurekebisha mtindo wa maisha. Amesema kuwa Mwenyezi Mungu ameumba mfumo wa uwepo wa mwanadamu kwa namna ambayo katika kipindi fulani cha mwaka huhitaji mabadiliko katika namna ya kuishi na kula; mabadiliko ambayo hupelekea kuinuka kwa roho na kuimarika kwa irada. Ramadhani ni uwanja wa mazoezi ya ibada na kujijenga nafsi, na kwa tafsiri nyingine ni hundi nyeupe yenye saini ya Kimungu kwa ajili ya msamaha na kuangazwa kwa nyoyo.
-
Sepah: Njama za Adui Kuangusha Mfumo wa Uongozi wa Kiislamu Zashindwa kwa Busara ya Kiongozi Mkuu wa Iran na Uangalifu wa Wananchi
Jenerali Naeini amesema tangu 13 Juni 2025 adui alilenga kuuangusha mfumo wa Kiislamu wa Iran kwa kusababisha machafuko ya kijamii, lakini kwa busara ya Kiongozi Mkuu Sayyid Ali Khamenei (h.a.) na uangalifu wa wananchi, njama hizo zilivunjika. Pia katika ghasia za 8 Januari 2026 na operesheni ya “Ahadi ya Kweli”, juhudi za adui zilikabiliwa na kushindwa kabisa.
-
Sayyid Ali Khamenei: "Hatua Ndogo Zenye Nia Njema Zinaweza Kubadilisha Historia"
Sayyid Ali Khamenei anasisitiza kwamba maisha ya mtu binafsi, hata kama yanaonekana ya kawaida, yana thamani zaidi kuliko maisha ya viongozi wakuu wa dunia. Maisha haya yamejaa matendo, nia njema, na shauku ambazo zinaweza kuwa na nguvu ya kubadilisha historia. Kauli hii inahimiza kila mtu kutambua uhamasisho na mchango wake binafsi katika jamii.
-
Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS): Vijana Wakumbushwa Wajibu wa Kuijenga Jamii ya Uadilifu katika Kipindi cha Ghaiba
Katika mnasaba wa maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS), Waislamu wa Shia na Sunni walikusanyika kujadili kuhusu Mwokozi wa Ulimwengu na wajibu wa Waumini katika kipindi cha Ghaiba. Khatibu Sheikh Suleimani Abdully aliwakumbusha vijana juu ya umuhimu wa kumcha Mwenyezi Mungu, kushukuru neema Zake na kujenga tabia njema ili kuandaa jamii yenye utu, uadilifu na iliyoepukana na dhulma na ufisadi.
-
Shahidi Sajad Zabihi: Alijitoa Muhanga Kulinda Usalama wa Wananchi wa Maeneo yenye uhitaji (Vijijini)
Wananchi na viongozi mbalimbali wamemuenzi Shahidi Zabihi kama shujaa wa taifa aliyesimama kulinda heshima, usalama na ustawi wa jamii. Tukio hilo limeacha huzuni kubwa, lakini pia limeongeza ari ya kulinda amani na mshikamano wa kitaifa.
-
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) Uturuki Yaionya Marekani: Imam Khamenei ni Mstari wetu Mwekundu
Jumuiya ya Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s) nchini Uturuki, katika tamko lake, imetangaza kuwa jaribio lolote la kumvunjia heshima au kumdhuru Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ni mstari mwekundu wa ulimwengu wa Kiislamu.
-
Sayyid Hassan Khomeini: Baraka za Mitume Ziko Katika Kuleta Maana Maishani mwa Binadamu
Kiongozi wa Haram ya Imam Khomeini (r.a) Asema: “Yesu (a.s), Mtume Muhammad (s.a.w), Amirul Mu’minin Ali (a.s) na wateule wote wa Mungu ni wenye baraka, kwani hutoa maana katika maisha ya binadamu. Ikiwa Mungu ataondolewa katika maisha ya binadamu, binadamu atageuka kuwa kiumbe mkali na mnyama, hata chini ya kiwango cha wanyama.”
-
Ujumbe wa Hongera wa Rais Pezeshkian kwa Kiongozi wa Wakatoliki Duniani
Katika kuendeleza diplomasia ya kidini na kuimarisha maadili ya kuishi kwa amani kati ya wafuasi wa dini mbalimbali, Rais wa Jamhuri alitoa ujumbe rasmi wa pongezi kwa kiongozi wa Wakatoliki duniani, akisisitiza umuhimu wa kuheshimiana, mazungumzo ya kidini na mshikamano wa kibinadamu katika dunia ya leo.
-
Mkutano wa “Mbinu za Kutoa Vipengele vya Mtindo wa Maisha wa Ahlul-Bayt (a.s)” umefanyika katika shirika la habari la ABNA:
Wasemaji walisisitiza kwamba mtindo wa maisha wa Ahlul-Bayt ni dhana inayobadilika na haipaswi kuangaliwa kwa mtazamo wa kutobadilika
Mkutano maalum wa kuchambua mbinu za kisayansi za kufanikisha viashiria vya kweli vya mtindo wa maisha ya Kiislamu umefanyika katika shirika la habari la ABNA, ukiwahusisha wasomi wa madarasa ya dini na vyuo vikuu. Katika mkutano huo, hatua za utekelezaji wa mradi mkubwa wa mtindo wa maisha wa Ahlul-Bayt (a.s) zilikaguliwa kwa kina, huku pia changamoto zinazojitokeza katika kushughulikia masuala mapya katika viwanja vya kimataifa zikijadiliwa kwa uchambuzi wa kitaalamu. Washiriki walisisitiza umuhimu wa mbinu za kisayansi, utafiti wa kimfumo, na tafsiri ya kisasa katika kutambua na kutekeleza vipengele vya mtindo wa maisha wa Ahlul-Bayt, ili kuhakikisha kuwa dhana hizi zinafanikisha maisha ya kiroho, kijamii na kitamaduni kwa njia inayofaa kwa muktadha wa sasa na mahitaji ya jamii za kisasa. Mkutano huu uliwezesha pia kubadilishana mawazo kati ya watafiti wa dini na wanasayansi, kwa lengo la kuunda vifaa vya kisayansi na miongozo thabiti kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa mtindo wa maisha wa Kiislamu na Ahlul-Bayt (as).
-
Mtindo wa Maisha wa Fatima (a.s) na Kauli “Jirani Kwanza Kisha Nyumba”: Kigezo cha Kiungu Kukabiliana na Ubinafsi wa Kisasa
Katika kuelekea kumbukizi ya kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (a.s), kikao cha kisayansi kuhusu “Mtindo wa Maisha wa Fatima na Mafundisho ya al-jār thumma al-dār (Jirani Kwanza Kisha Nyumba)” kiliandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Habari la ABNA, ambapo watafiti walibainisha changamoto za familia katika enzi ya kisasa—hususan mgongano kati ya fikra za kisasa na mwenendo wa kimapokeo. Katika kikao hicho, mfano wa Maisha wa Bibi Zahra (a.s) uliwasilishwa kama muongozo wa kiungu na wa vitendo unaojenga maadili ya kuwajali wengine na kuleta mizani kati ya haki na wajibu ndani ya familia.
-
Mwigizaji wa Australia Aukosoa Vikali Utawala wa Kizayuni kwa Kutojali Maisha ya Wapalestina
Amesema: “kila siku nashuhudia dharau na kutojali maisha ya Wapalestina kwa upande wa Waisraeli,” akieleza kuwa mwenendo huo ni “wa aibu” na kwamba wale wanaotekeleza “matendo haya mabaya” wanairudisha nyuma ubinadamu kila siku.
-
Kufungwa kwa Uwanja wa Ndege wa Sana’a kumeweka maisha ya maelfu ya wagonjwa katika hatari
Kwa kuendelea kwa mzingiro na kusitishwa kwa shughuli za Uwanja wa Ndege wa Sana’a, maelfu ya wagonjwa wa Yemen wamenyimwa upatikanaji wa dawa na fursa ya kutibiwa nje ya nchi.
-
Mtindo wa Maisha | Ushauri / Wasia wa Kutoa Chakula Kuwalisha Watu
“Iwapo nyinyi mmekula na hamuhitaji, basi kuna watu wanaohitaji. Wapeni wao haya matunda badala ya kuyapoteza".
-
Nafasi ya Kupuuzia Mambo ya Kimaada na Thamani za Uongo katika Ndoa
Ndoa ya Bibi Fatima (a.s) na Amirul-Mu’minin Ali (a.s) ni kigezo cha pekee kinachoonyesha jinsi ambavyo mambo ya kimaada na thamani za uongo yalipuuzwa kabisa. Uteuzi wa mwenzi wa maisha ulitokana na taqwa, imani na maadili, si utajiri wala muonekano wa nje. Kwa kuishi kwa urahisi, unyenyekevu na mbali na anasa, walijenga nyumba iliyojaa utulivu, baraka na uimara wa kiroho. Mtindo huu wa maisha unatupa ujumbe wazi: ukombozi kutoka katika pupa ya mali na mapambo ndiyo njia ya kufikia furaha ya kweli katika maisha ya ndoa.
-
Picha kuhusu mradi wa fani ya ushonaji kwa ajili ya Palestina katika Msikiti wa Afrika Kusini
Baadhi ya wanaharakati na wafuasi wa Palestina nchini Afrika Kusini wanashona vipande vya kitambaa vyenye rangi za bendera ya Palestina, kuunda kazi ya ishara ya kumbukumbu kwa watoto waliopoteza maisha katika vita vya Ghaza. Kazi hii itafunguliwa rasmi mnamo tarehe 29 Novemba, Siku ya Kimataifa ya Umoja na Palestina.
-
Bibi Zahra (a.s): Kielelezo cha Juu cha Maadili ya Kibinadamu na Kiislamu Kuhusu Mwanamke
Bibi Zahra (a.s) ni kielelezo cha Mwanamke kamili katika Uislamu - mfano wa ucha Mungu, hekima, upendo wa kifamilia, ushujaa wa kijamii na mapambano ya kiroho. Maisha yake ni dira ya kudumu kwa wanawake na wanaume wote wanaotaka kufikia ukamilifu wa kibinadamu katika njia ya Mwenyezi Mungu.
-
Janga la Kibinadamu Gaza; Watoto Yatima Katika Hali ya Ndoto Mbaya
Janga la kibinadamu katika Ukanda wa Gaza limeharibu maisha ya maelfu ya watoto. Watoto hawa wamekuwa wakikabiliana na hali ya kukimbia, njaa, kifo cha wapendwa, na vurugu za kutisha kwa takriban miaka miwili. Ripoti zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 65,000 wamefariki Gaza, huku maelfu ya watoto wakipoteza wazazi wao. Hali hii ya ukosefu wa usalama na mahitaji ya msingi inatengeneza athari kubwa za kimahusiano na kisaikolojia kwa vizazi vijavyo, na kufanya msaada wa haraka wa kimataifa kuwa jambo la dharura. Watoto hawa yatima sasa wanahitaji hifadhi, chakula, huduma za afya na msaada wa kisaikolojia ili kuweza kuendelea na maisha yao.
-
Vifo vya Wapalestina 453, wakiwemo watoto 150, vimeripotiwa kutokana na njaa na utapiamlo huko Gaza
Wizara ya Afya ya Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa idadi ya waathirika waliopoteza maisha kutokana na njaa na utapiamlo imefikia watu 453, ambapo miongoni mwao wako watoto 150.
-
Darasa la Qur’an Tukufu katika Madrasat ya Mabanati ya Hazrat Zainab (sa) Laendelea kwa Mafanikio Makubwa
Darsa hili la Qur’an Tukufu linawafundisha zaidi Wanafunzi kuwa Qur'an ni mshirika na muombezi wa yeyote mwenye kushikamana nayo Siku ya Kiyama, hummulikia njia yake hapa duniani, na humuinua katika ngazi za juu Peponi
-
Zaidi ya Wanawake na Wasichana 1,000 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
UN: Wanawake na Wasichana 1,025 Wamefariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan. Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) nchini Afghanistan imetangaza kuwa: Jumla ya wanawake na wasichana 1,025 wamepoteza maisha kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea katika maeneo ya mashariki mwa Afghanistan. Taarifa hiyo inasisitiza ukubwa wa athari za kibinadamu, hasa kwa wanawake na watoto, katika tukio hili la maafa ya asili.
-
Maneno Mafupi, Yenye Maana Pana:
Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha: "Kuwa na mzigo mwepesi ili mfike (kwenye safari yenu)!"
تَخَفَّفُوا تَلْحَقُوا، فَإِنَّمَا يُنْتَظَرُ بِأَوَّلِكُمْ آخِرُكُمْ "Punguzeni mizigo ili mfike (kwenye malengo ya safari yenu), kwa maana waliotangulia wanawasubiri mlio nyuma." Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha – Mtazamo wa Akhera katika Jitihada za Binadamu: Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha inaangazia maisha ya binadamu kwa mtazamo wa akhera, na inaeleza kwamba: Binadamu anapaswa kuwa mwepesi wa mizigo (wa kidunia), ili aweze kwa urahisi kutoka duniani na kuelekea kwenye maisha ya akhera. Hili linaonyesha kuwa jitihada za binadamu si kwa ajili ya dunia pekee, bali kwa ajili ya ukamilifu wa kiutu (kamilifu) na maisha ya milele.
-
Mwakilishi wa Kiongozi Mkuu wa Kidini katika masuala ya Hija na Ziara:
"Kufuata mtindo wa maisha wa Imam Hussein (a.s) ni suluhisho kwa changamoto za jamii ya leo"
Mwakilishi wa Kiongozi Mkuu wa Kidini katika Masuala ya Hija na Ziara, katika hafla ya kufunga tukio la pili la kimataifa la vyombo vya habari “Nahnu Abna’ Al-Husayn (a.s)”, alisisitiza umuhimu wa kunufaika na mtindo wa maisha na mafundisho ya Imam Husayn (a.s) ili kujibu mahitaji ya jamii ya leo.
-
Kuongezeka kwa Idadi ya Mashahidi wa Njaa Gaza hadi 269
Wizara ya Afya ya Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa katika saa 24 zilizopita watu wengine watatu wamepoteza maisha yao kutokana na njaa na ukosefu wa chakula.
-
Chuo Kikuu cha al-Mustafa (s) Dar es Salaam - Tanzania Chaandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu: "Dakika za Mwisho za Maisha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)"
Mtoa Mada: Sheikh Taqi Zakariya. Tarehe: Jumamosi, 16-08-2025. Muda: Kuanzia Saa 4:00 Ask Asubuhi hadi 6:00 Mchana. Eneo: Muswalla wa Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam. Mwaliko huu ni kwa Wote.
-
Magharibi mwa Asia na Mashariki ya Kati | Watu 11 Wauawa na Kujeruhiwa Kutokana na Mlupuko wa Mabomu Yaliyosalia huko Tyre, Lebanon
Watu 11 wa jeshi la Lebanon wameuawa na kujeruhiwa kufuatia mlipuko wa mabomu yaliyosalia kutoka kwenye uvamizi wa awali wa utawala wa Kizayuni kusini mwa Lebanon, tukio ambalo limepelekea viongozi wa juu wa nchi hiyo kutuma salamu za rambirambi.
-
Makamu wa Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Kishia Lebanon Aikosoa Vikali Serikali ya Nchi Hiyo
Alielekeza maneno yake kwa Rais Joseph Aoun, akisema: "Uliwaambia watu wa Muqawama kuwa waitegemee Serikali – lakini haukusema ni Serikali ipi hiyo? Watu wetu hawako tayari kuwa wahanga wa wauaji ambao watawatendea kama walivyowatendea Wapalestina."
-
(Muqawamah) Kusimama dhidi ya Ubeberu ni Fahari ya Mataifa ya Waumini
"Kazi yetu kuu ni kuinua bendera ya Qur’an ili kwa kueneza mtindo sahihi wa maisha, jamii ya Kiqur’ani iweze kuundwa. Ikiwa nchi za Kiislamu zitaifuata Qur’an, zitauweza kuwalazimisha maadui kurudi nyuma"
-
Wataalamu wa Kieneo katika Mahojiano na ABNA: Njaa ya kimfumo dhidi ya watu wa Gaza ni uhalifu usio na kifani na doa la aibu juu ya uso wa Binadamu
Jinai za uharibifu kamili wa ardhi, watu na kila dalili za maisha katika ardhi za Palestina inayokaliwa kwa mabavu (na Utawala wa Kizayuni) zinaakisi matamanio ya jeshi la Netanyahu kuwa tawi la uhalifu wa kimataifa katika ardhi za Kiislamu.
-
Falsafa ya Maombolezo na Kumbukumbu ya A'shura | Kulinda Haki na Uhuru wa Watu ni Muhimu zaidi kuliko Maisha binafsi
Haki ya mtu binafsi na umma: Imam Hussein alijua kwamba alikuwa akielekea kifo, lakini alikusudia kuonyesha ulimwengu kuwa kulinda haki na uhuru wa watu ni muhimu kuliko maisha binafsi. Maombolezo ya Ashura yanatufundisha kuwa watu wanapaswa kuwa tayari kujitolea, si tu kwa ajili ya nafsi zao, bali kwa ajili ya ustawi wa jamii.