Nchi
-
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran Wachapisha Picha za Hangar za Ndege za Kivita za Marekani Zilizoharibiwa Nchini Jordan
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wamechapisha picha zinazoonyesha uharibifu mkubwa katika hangar za ndege za kivita za Marekani aina ya F-15 na F-16 katika kituo cha kijeshi cha Marekani nchini Jordan, kufuatia shambulizi la makombora na ndege zisizo na rubani.
-
Jeshi la Iran Laangusha Ndege Isiyo na Rubani ya Adui Kusini mwa Nchi
Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuangamiza ndege isiyo na rubani ya adui aina ya “Lukas” kwa kutumia mifumo ya ulinzi wa anga ya Jeshi la Wanamaji kusini mwa nchi.
-
Iran: Kuwaadhibu waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi ni haki ya taifa
Naibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa kuwawajibisha waliopanga, kutekeleza na kushiriki katika mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu pamoja na mashahidi wengine ni haki halali ya taifa la Iran.
-
Rais Pezeshkian: Sera za Kivamizi za Utawala wa Kizayuni Ndizo Chanzo cha Ukosefu wa Usalama katika Eneo
Rais Masoud Pezeshkian amesema sera za uchokozi za utawala wa Kizayuni ndizo chanzo kikuu cha ukosefu wa usalama katika eneo, huku Iran na Serbia zikisisitiza umuhimu wa kuimarisha amani, utulivu na ushirikiano wa pande mbili.
-
Iran na Urusi Zakubaliana Kurahisisha Biashara na Kuimarisha Ushirikiano wa Kibenki
Marais wa Benki Kuu za Iran na Urusi wamehimiza kuimarishwa kwa ushirikiano wa kifedha, kupanuliwa kwa biashara baina ya nchi hizo mbili, na kuendelezwa kwa Mradi wa Ukanda wa Kaskazini (North Corridor) ili kurahisisha miamala ya kiuchumi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Mabalozi wa Nchi za Amerika ya Kusini mjini Tehran
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amekutana na mabalozi wa nchi za Amerika ya Kusini mjini Tehran na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Iran na mataifa hayo, huku mabalozi wa Uruguay na Brazil wakimzawadia jezi za timu zao za taifa kama ishara ya urafiki.
-
Kamanda wa Majeshi ya Ardhi ya Iran: Tumejiandaa Kujibu kwa Uamuzi Vitisho Vyovyote
Kamanda wa Majeshi ya Ardhi ya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Ali Jahanshahi, amesema kuwa vikosi vya nchi hiyo vilivyoko mpakani viko katika utayari kamili wa kioperesheni na vimejiandaa kukabiliana kwa uthabiti na vitisho vyovyote vinavyoweza kujitokeza.
-
Mkurugenzi Mkuu wa IRNA: Sehemu ya Migongano ya Dunia Leo Inaendeshwa Kupitia Vita vya Maarifa na Simulizi
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRNA), Hussein Jaberi Ansari, amesema kuwa vyombo vya habari vimekuwa nguzo muhimu ya nguvu, ushawishi na hata usalama wa taifa, huku akisisitiza kuwa sehemu kubwa ya migongano ya dunia inaendeshwa kupitia vita vya kiakili na mapambano ya simulizi.
-
Iran Yaikosoa Rasimu ya Azimio la Marekani katika Baraza la Magavana wa IAEA, Yataja Kuwa ya Kisiasa na ya Uchochezi
Iran imeeleza kuwa rasimu ya azimio iliyowasilishwa na Marekani pamoja na Uingereza, Ufaransa na Ujerumani katika Baraza la Magavana la Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ni ya kisiasa na ya uchochezi, ikidai kuwa inalenga kuhamisha lawama kutoka kwa washambuliaji kwenda kwa mhanga.
-
Reuters Yadai Marekani Inatafakari Kutumia Mali za Iran Zilizozuiwa Kufadhili Ukarabati wa Uharibifu katika Nchi za Kiarabu
Reuters imedai kuwa Marekani inazingatia uwezekano wa kutumia mali za Iran zilizozuiwa kufadhili ukarabati wa uharibifu wa vita katika baadhi ya nchi za Kiarabu za Ghuba.
-
Nchi Wanachama wa D-8 Zakubaliana Kupanua Ushirikiano wa Nishati Kupitia Azimio la Baku
Mawaziri na wawakilishi wa nchi wanachama wa D-8 wamepitisha Azimio la Baku, wakisisitiza kuimarisha ushirikiano katika usalama wa nishati, nishati jadidifu na maendeleo ya miundombinu ya pamoja ili kukabiliana na changamoto za sasa za sekta ya nishati duniani.
-
Mzozo wa Urani Wazidi Kutatiza Makubaliano Kati ya Iran na Marekani
Ripoti zinaeleza kuwa Iran inaendelea kusimama kidete katika msimamo wake wa kutoruhusu akiba yake ya urani iliyorutubishwa kuhamishwa nje ya nchi, jambo linaloongeza ugumu katika mazungumzo yanayoendelea na Marekani kuhusu makubaliano mapya ya nyuklia na usalama wa kikanda.
-
CNN: Trump Ametishia au Kushambulia Taifa Moja Kati ya Kila Mataifa 13 Duniani
Ripoti ya CNN imesema matamshi ya Donald Trump kuhusu kuitishia Oman kwa mashambulizi yameongeza wasiwasi wa kimataifa kuhusu matumizi ya vitisho vya kijeshi katika sera za nje za Marekani na athari zake kwa usalama wa dunia.
-
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje kuhusu kuongezeka kwa mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan
Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikieleza wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan. Iran imezitaka pande zote mbili kuanza mazungumzo ya haraka ili kusitisha mapigano, kuheshimu mamlaka na mipaka ya kila nchi, na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza hali ya taharuki. Pia imetangaza utayari wake kusaidia juhudi za kupunguza mvutano na kufanikisha maelewano ya amani.
-
Mkurugenzi wa Channel 12 Israel alishangazwa ghafla kumsikia Dereva wa lori wa Iran akisema: "I LOVE YOU KHAMENEI!"
Dereva wa lori wa Iran alishangaza Channel 12 Israel kwa kusema kuwa Iran ni nchi bora aliyowahi kuzuru na akamtaja Khamenei kwa upendo: "I LOVE YOU KHAMENEI!"
-
Sepah: Njama za Adui Kuangusha Mfumo wa Uongozi wa Kiislamu Zashindwa kwa Busara ya Kiongozi Mkuu wa Iran na Uangalifu wa Wananchi
Jenerali Naeini amesema tangu 13 Juni 2025 adui alilenga kuuangusha mfumo wa Kiislamu wa Iran kwa kusababisha machafuko ya kijamii, lakini kwa busara ya Kiongozi Mkuu Sayyid Ali Khamenei (h.a.) na uangalifu wa wananchi, njama hizo zilivunjika. Pia katika ghasia za 8 Januari 2026 na operesheni ya “Ahadi ya Kweli”, juhudi za adui zilikabiliwa na kushindwa kabisa.
-
Mwendesha Mashtaka wa Tehran afungua mashtaka dhidi ya wanasiasa wanaounga mkono mikondo hasimu
Mwendesha Mashtaka wa Tehran ametangaza mashtaka dhidi ya baadhi ya wanasiasa kwa tuhuma za kushirikiana na Marekani na utawala wa Kizayuni, ambapo watu 4 wamekamatwa kwa madai ya kuchochea vurugu na kudhoofisha usalama wa ndani.
-
Rais wa Azerbaijan: Hatutumi vikosi vya kulinda amani Gaza
Ilham Aliyev, Rais wa Azerbaijan, ametangaza kuwa nchi yake haina mpango wa kutuma vikosi vyake kushiriki katika operesheni za kulinda amani nje ya mipaka ya nchi, ikiwemo Gaza.
-
Mkutano wa dharura wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kujadili na kukabiliana na mradi wa Israel kuhusu Somalia
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, katika mkutano wa dharura uliofanyika leo Jumapili nchini Misri, imeitikia hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kulitambua eneo la Somaliland, na ikaeleza kuwa hatua hiyo ni tishio kwa usalama wa kikanda na ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.
-
Ufichuzi wa mtandao wa Kizayuni:
Israel imekubali kuitambua Somaliland kwa masharti ya kukubali kuwapokea wakazi wa Gaza!
Jana, Benjamin Netanyahu, Gideon Sa’ar Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni, pamoja na Abdirahman Mohamed Abdullahi, rais wa kujitangaza wa Somaliland, walitia saini tamko la pamoja la kuitambua Somaliland kama nchi huru na inayojitegemea.
-
Naibu Kamanda wa Vikosi vya Nchi Kavu vya Jeshi la Iran: Hatutakuwa waanzilishi wa mashambulizi kamwe
Naibu Kamanda wa Vikosi vya Nchi Kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa jeshi halitakuwa kamwe mwanzilishi wa mashambulizi, akieleza kuwa lengo la kuimarisha jeshi sio vita, bali ni kuzuia vita na kujenga uwezo wa kuzuia (deterrence).
-
Turki Al-Faisal: Tishio Kuu la Mashariki ya Kati Sio Iran, Bali ni Israel
Shambulizi Dhidi ya Ujumbe wa Hamas Qatar ni Onyo kwa Nchi za Ghuba | Katika kauli yake nzito, Turki Al-Faisal pia amebainisha kuwa shambulizi la Israel dhidi ya ujumbe wa Hamas nchini Qatar lilikuwa ujumbe wa vitisho kwa nchi za Ghuba, akisema hatua hiyo ilikuwa onyo la wazi kuwa mataifa ya Ghuba yako katika hatari na yanapaswa kuchukua tahadhari za pamoja za kiulinzi.
-
Dkt. Khamehyar: Uturuki ya baadae haitakwenda kuelekea Uislamu wa kisiasa wa kiwango cha juu, wala haitarudi kwenye msimamo mkali wa kisekula
Mshauri wa masuala ya kimataifa wa Chuo Kikuu cha Dini na Madhehebu: Kudumu kwa chama cha AKP kwa kipindi cha miaka ishirini iliyopita kumebadilisha kabisa sura ya Uislamu wa kisiasa nchini Uturuki. Ushindani kati ya Waislamu wa kisiasa na wasekula utaendelea.
-
Mahakama ya Juu ya Iraq yavunja Bunge / Hadi kuundwa kwa Baraza jipya la Mawaziri, Serikali itakuwa tu ya “kusimamia mambo ya kila siku”
Mahakama Kuu ya Shirikisho ya Iraq imetangaza rasmi kumalizika kwa muhula wa tano wa Bunge la nchi hiyo, na kuitaja serikali ya sasa kuwa ni “serikali ya kusimamia mambo ya kila siku”, yenye mamlaka tu katika kushughulikia masuala ya kawaida na yasiyoweza kuahirishwa.
-
Mufti wa Oman ametoa wito kwa nchi za Kiislamu kusimama imara dhidi ya ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano Ghaza na Israeli
Sheikh Ahmed bin Hamad Al-Khalili, Mufti Mkuu wa Oman, kwa kushangaza hatua za utawala wa Kizayuni za kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano Ghaza, kupitia tamko lililotolewa, aliwahimiza jamii ya kimataifa na nchi za Kiislamu kulazimisha utawala wa Kizayuni kuheshimu makubaliano na kudumisha amani ya kusitisha mapigano.
-
Sayyid Ali Khomeini: “Kama Ubalozi wa Marekani usingelivamiwa, leo tusingekuwa na Makombora wala ishati ya nyuklia"
Akiisisitizia kauli kwamba “uvamizi wa ubalozi wa Marekani uliimarisha uhuru wa Iran,” alisema: “Kama tukio hilo lisingetokea, leo hii Jamhuri ya Kiislamu isingekuwepo, na nchi yetu isingepata teknolojia ya makombora na nishati ya nyuklia, kwani Marekani ilikuwa inapinga maendeleo haya.”
-
Je, Israil ni Nchi Huru au ni Jimbo linalotawaliwa na Marekani?
Kadiri ushawishi wa Marekani katika maamuzi ya Israil unavyozidi kufichuka, mijadala imeibuka ndani ya duru zisizo rasmi za utawala wa Kizayuni ikiuliza: “Je, Israil kweli ni nchi huru au ni jimbo linalotawaliwa na Marekani?” Zeev Elkin, Waziri wa Masuala ya Yerusalemu wa utawala wa Kizayuni, alijibu ukosoaji huu kwa kusema katika mahojiano ya vyombo vya habari kwamba uhusiano wa Israil na Marekani ni “ushirikiano wa kimkakati, si utegemezi.”
-
Mwanachama wa zamani wa Baraza la Kitaifa la Palestina azungumza na ABNA:
Kuwanyang’anya silaha wamiliki halali wa ardhi ya Palestina ni kuwapendelea kabisa wavamizi / Umuhimu wa Kuamka kwa dhamiri za tawala za Kiarabu
Dkt. Rabhiy Halloum amesisitiza kuwa uamuzi wa kweli wa kisiasa na kuamka kwa dhamiri za nchi za Kiarabu ndiko kutakakoamua mustakabali wa ukombozi wa Palestina na kulinda amani ya kudumu katika eneo lote la Mashariki ya Kati.
-
Nafasi ya Marājiʿ wa Kishia katika Kulinda Umoja wa Ardhi na Utambulisho wa Kitaifa- Sehemu ya 2 | Marāji ni, Walinzi wa Uhuru wa Nchi za Kiislamu
Mfano mashuhuri ni Ayatullah al-Uzma Sayyid Muhammad Hasan Shirazi, ambaye alitoa Fat'wa maarufu ya kupiga marufuku tumbaku mwaka 1891 huko Iran, hatua iliyozuia njama za kikoloni za Waingereza na kuwa alama ya mapambano ya Kiislamu dhidi ya ukoloni. Vivyo hivyo, Ayatullah Kashif al-Ghita, Ayatullah Muhsin al-Hakim, na Imam Khomeini (r.a) walikuwa mstari wa mbele katika kuhimiza mapambano ya kulinda utu, uhuru, na heshima ya mataifa ya Kiislamu.
-
Magaidi 10, Wakiwemo Wanawake Wawili, Watekwa na Shirika la Taarifa za Kijajusi la Kijeshi la Iraq
Shirika la Taarifa za Kijeshi la Iraq leo limetangaza kuwa katika operesheni mbalimbali za kiusalama, limefanikiwa kuchukua watu 10 wa kigaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi, wakiwemo wanawake 2.