ndege
-
Walinzi wa Mapinduzi wa Iran Wawashukuru Wananchi wa Jordan na Kutangaza Kulenga Ndege za Marekani Katika Uwanja wa Ndege wa Aqaba
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wamewashukuru wananchi na wanajeshi wa Jordan kwa taarifa walizodai zilisaidia katika mashambulizi dhidi ya vituo vya Marekani, huku wakitangaza kulenga ndege za kijeshi za Marekani katika Uwanja wa Ndege wa Aqaba.
-
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran Wachapisha Picha za Hangar za Ndege za Kivita za Marekani Zilizoharibiwa Nchini Jordan
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wamechapisha picha zinazoonyesha uharibifu mkubwa katika hangar za ndege za kivita za Marekani aina ya F-15 na F-16 katika kituo cha kijeshi cha Marekani nchini Jordan, kufuatia shambulizi la makombora na ndege zisizo na rubani.
-
Vyombo vya Habari vya Iran: Picha za Satelaiti Zathibitisha Uharibifu wa Hangar ya Ndege za Kivita katika Kambi ya Muwafaq Al-Salti Jordan
Vyombo vya Habari vya Iran vimeripoti kuwa picha za satelaiti zinaonyesha shambulizi la usahihi lililosababisha kuharibiwa kwa hangar ya ndege za kivita katika Kambi ya Muwafaq Al-Salti nchini Jordan, ambako kuna wanajeshi wa Marekani.
-
Marekani yaiondoa ndege yake ya upelelezi MQ-4C Triton kutoka Jordan kuelekea Italia baada ya mashambulizi ya Iran
Ripoti zinaeleza kuwa Marekani imeiondoa ndege yake ya kisasa ya upelelezi aina ya MQ-4C Triton kutoka Jordan na kuihamishia Italia, hatua inayokuja baada ya mashambulizi ya Iran dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Ansarallah yaonya kulenga miundombinu muhimu ya Saudi Arabia katika hatua yake ijayo
Mwanachama wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarallah ya Yemen, Mohammed al-Bukhaiti, amesema kuwa miundombinu muhimu ya Saudi Arabia inaweza kulengwa katika majibu yao yajayo, akieleza kuwa maeneo hayo yanachukuliwa kuwa malengo halali kwa mujibu wa msimamo wa harakati hiyo.
-
Iran yadai kuidungua droni ya Marekani aina ya MQ-1 katika Mlango wa Hormuz
Iran imedai kuwa imeidungua droni ya kijeshi ya Marekani aina ya MQ-1 iliyokuwa ikiruka katika eneo la Mlango wa Hormuz, huku mamlaka za Marekani zikiwa hazijatoa uthibitisho wa madai hayo.
-
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian Awasili Najaf Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Najaf nchini Iraq kwa ajili ya kushiriki katika mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ambapo alipokelewa na Waziri Mkuu wa Iraq pamoja na viongozi wengine waandamizi wa nchi hiyo.
-
IRGC Yatangaza Kuiangusha Ndege ya Marekani Isiyo na Rubani Aina ya MQ-9 Kusini mwa Iran
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limeiangusha ndege ya Marekani isiyo na rubani aina ya MQ-9 katika anga ya mji wa Khormuj, mkoani Bushehr, kufuatia kile ilichokitaja kuwa mashambulizi ya anga ya Marekani.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Uwezo wa Ulinzi wa Taifa Hauko Kwenye Majadiliano
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Ebn al-Reza, amesema uwezo wa Iran katika sekta ya ulinzi, makombora na ndege zisizo na rubani ni sehemu ya usalama wa taifa na hauwezi kujadiliwa katika mazungumzo yoyote.
-
IRGC Yadai Kuilenga na Kuiangusha Ndege Ndege Isiyo na Rubani ya Marekani MQ-9 Nchini Bushehr
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) wametangaza kuuangusha ndege isiyo na rubani ya kijeshi ya Marekani aina ya MQ-9 katika Mkoa wa Bushehr kusini mwa Iran.
-
Iran Yatangaza Mashambulizi ya Kulipiza Kisasi Dhidi ya Malengo ya Marekani katika Ghuba ya Uajemi
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran limesema limejibu mashambulizi ya Marekani kwa kulenga kambi za kijeshi na makao makuu ya US Fifth Fleet, huku likionya kuwa usalama wa Mlango wa Hormuz ni mstari mwekundu ambao ukiukwa utakuwa na gharama kubwa.
-
IRGC Yatangaza Mashambulizi ya Kulipiza Kisasi Dhidi ya Kambi ya Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limesema limelenga kambi ya kijeshi ya Marekani baada ya shambulizi lililoripotiwa kufanywa karibu na Uwanja wa Ndege wa Bandar Abbas, likionya kuwa uchokozi wowote dhidi ya Iran utakabiliwa na majibu makali zaidi.
-
IRGC: Ndege za Marekani za RQ-4 na F-35 Zalikimbia Baada ya Kujibiwa na Ulinzi wa Anga wa Iran
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kudungua ndege isiyo na rubani ya Marekani aina ya MQ-9 na kulazimisha ndege ya RQ-4 pamoja na ndege ya kivita ya F-35 kuondoka katika anga ya Iran baada ya kujibiwa na mifumo ya ulinzi wa anga. IRGC imeonya kuwa uvunjaji wowote wa usitishaji mapigano utakabiliwa na majibu makali ya kulipiza kisasi.
-
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq: Wavamizi wa Marekani Lazima Waondoke
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq imesisitiza katika taarifa yake kwamba uwepo wa majeshi ya Marekani nchini Iraq ni aina ya uvamizi unaokiuka mamlaka ya taifa hilo, na imetaka kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani kutoka ardhi ya Iraq. “Wavamizi wanaendelea kukiuka anga la Iraq; iwe kupitia ndege zisizo na rubani (drones) au kwa kutumia ndege zao za kivita. Hatua hizi zinachukuliwa kuwa tishio kubwa kwa usalama, uthabiti na umoja wa ardhi ya nchi, na ni uvamizi wa wazi dhidi ya mamlaka na heshima ya dola ya Iraq.”
-
Sepah: Njama za Adui Kuangusha Mfumo wa Uongozi wa Kiislamu Zashindwa kwa Busara ya Kiongozi Mkuu wa Iran na Uangalifu wa Wananchi
Jenerali Naeini amesema tangu 13 Juni 2025 adui alilenga kuuangusha mfumo wa Kiislamu wa Iran kwa kusababisha machafuko ya kijamii, lakini kwa busara ya Kiongozi Mkuu Sayyid Ali Khamenei (h.a.) na uangalifu wa wananchi, njama hizo zilivunjika. Pia katika ghasia za 8 Januari 2026 na operesheni ya “Ahadi ya Kweli”, juhudi za adui zilikabiliwa na kushindwa kabisa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mnamo tarehe 22 Bahman, kwa kuonesha dhamira na msimamo wenu thabiti, muwavunje moyo maadui
Kiongozi wa Mapinduzi amesema kuwa ushiriki wa wananchi katika maandamano ya tarehe 22 Bahman na kuonyesha utii kwa Jamhuri ya Kiislamu ni silaha muhimu ya kuwarudisha nyuma maadui wanaolenga Iran na maslahi ya taifa. Amefafanua kuwa nguvu ya taifa haitokani zaidi na makombora au ndege za kivita, bali inatokana na umoja, fikra, azma na msimamo thabiti wa wananchi.
-
Kukamatwa kwa mtuhumiwa wa kushiriki katika mauaji ya Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah
Mwandishi wa habari wa Lebanon ametangaza kuwa mtu aliyeko chini ya ulinzi wa Idara ya Usalama wa Umma ya Lebanon alihusika kwa kushirikiana na Israel na kukusanya taarifa zilizopelekea kuuawa kwa Sayyid Hassan Nasrallah.
-
Kituo cha 12 cha Israel: "Hezbollah ina wapiganaji 70,000 na mamia ya makombora, iko tayari kwa makabiliano na Israel"
Usiku uliopita, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Lebanon, utawala huo ulianzisha mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya Lebanon.
-
Ukraine Yashambulia Makaazi ya Putin kwa Ndege Droni 91 / Trump Ashtuka
Ikulu ya Kremlin jioni ya Jumatatu ilitangaza kuwepo kwa mawasiliano ya simu kati ya marais wa Urusi na Marekani, na kubainisha kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alishtushwa na shambulio la ndege zisizo na rubani (droni) la Ukraine dhidi ya makaazi ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin.
-
Kutua kwa Ndege ya Elfu Moja Iliyobeba Silaha katika Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion huko Tel Aviv
Ndege ya elfu moja iliyobeba silaha na rasilimali za kijeshi tangu kuanza kwa vita vya Gaza, kama sehemu ya daraja kubwa la anga la Israel, imepataja kwenye uwanja wa ndege wa Ben-Gurion.
-
Kufungwa kwa Uwanja wa Ndege wa Sana’a kumeweka maisha ya maelfu ya wagonjwa katika hatari
Kwa kuendelea kwa mzingiro na kusitishwa kwa shughuli za Uwanja wa Ndege wa Sana’a, maelfu ya wagonjwa wa Yemen wamenyimwa upatikanaji wa dawa na fursa ya kutibiwa nje ya nchi.
-
Italia na Hispania Zimetuma Manowari za Kivita kwa ajili ya Kulinda Msafara wa Meli za Sumuud
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.
-
-
Jeshi la Yemen Latangaza Awamu ya Nne ya Kufunga Njia za Baharini, Latoa Onyo kwa Ndege Zinazosaidia Israel
Ndege yoyote, iwe ya kijeshi au kibiashara, itakayojihusisha na shughuli za kusaidia Israel, tutaiangamiza. Itaingia kwenye historia.