Jenerali
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Vyombo vya Majini Vinavyotumika Dhidi ya Wananchi wa Iran Haviwezi Kupita Katika Bahari ya Hormuz
“Udhibiti wa Bahari ya Hormuz uko mikononi mwa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Vifaa vinavyotumika dhidi ya wananchi wa Iran haviwezi kupita katika Bahari ya Hormuz.”
-
Brigedia Jenerali Ibn al-Ridha: Vikwazo na Vita Vimekuwa Chachu ya Maendeleo ya Kiteknolojia ya Ulinzi Nchini Iran
Naibu Waziri wa Ulinzi na Msaada wa Majeshi ya Iran, Brigedia Jenerali Sayyid Majid Ibn al-Ridha, amesema vikwazo na vita vimekuwa miongoni mwa sababu zilizochochea maendeleo makubwa ya kiteknolojia katika sekta ya ulinzi ya Iran.
-
Kamanda wa Makao Makuu ya Pamoja ya Ulinzi wa Anga ya Iran: Kusasisha Uwezo na Mafunzo ni Lazima ili Kukabiliana na Maendeleo Mapya
Kamanda wa Makao Makuu ya Pamoja ya Ulinzi wa Anga nchini Iran, Brigedia Jenerali Alireza Elhami, amesema kusasisha vifaa, uwezo na mitaala ya mafunzo ni jambo la lazima ili kukabiliana na mabadiliko ya vitisho vya anga na maendeleo ya teknolojia za kijeshi.
-
Kamanda wa Walinzi wa Mipaka wa Iran awasili Pakistan kwa mkutano wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai
Kamanda wa Vikosi vya Walinzi wa Mipaka wa Iran, Brigedia Jenerali Ali Akbar Javidan, amewasili Islamabad kushiriki mkutano wa makamanda wa walinzi wa mipaka wa nchi wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO).
-
Brigedia Jenerali Ali Fadavi: Ushahidi wa Imam Shahidi Khamenei Umeufanya Njia ya Mapinduzi ya Kiislamu Kuwa Wazi Zaidi
Mkuu wa Kundi la Washauri wa Makao Makuu ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Ali Fadavi, amesema kuwa ujasiri ulikuwa sifa kuu ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei na kwamba ushahidi wake umeifanya njia ya Mapinduzi ya Kiislamu kuwa wazi zaidi.
-
Kamanda Abdollahi: Tutawalipiza Kisasi Waliomuua Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra)
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s), Luteni Jenerali Ali Abdollahi, amesema Iran itaendelea kufuatilia na kuwaadhibu waliomuua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi pamoja na mashahidi wengine.
-
Jenerali Qaani: Mazishi ya Sayyid Ali Khamenei Nchini Iraq Yataimarisha Umoja Dhidi ya Fitna na Kuhuisha Wito wa Haki
Kamanda wa Kikosi cha Quds amesema marasimu ya mazishi ya Sayyid Ali Khamenei nchini Iraq yataonyesha mshikamano wa wananchi wa Iraq na Iran, na kuimarisha msimamo wa pamoja dhidi ya fitna na migawanyiko.
-
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatamul Al-Anbiya Ampongeza Mohseni-Ejei kwa Kuteuliwa Tena Kuongoza Mhimili wa Mahakama
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s), Meja Jenerali Ali Abdollahi, amesema kutekeleza maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kuzingatia matarajio ya Kiongozi Shahidi kutahakikisha mafanikio endelevu ya Mkuu wa Mhimili wa Mahakama wa Iran.
-
Kiongozi wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (SAW): Vikosi vyetu vya ulinzi viko tayari kuimarisha mamlaka na usalama wa taifa
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (SAWW), Meja Jenerali Ali Abdullahi, amesema vikosi vya ulinzi vya Iran viko katika utayari wa hali ya juu kulinda usalama wa taifa, haki za wananchi na kukabiliana na vitisho vyovyote vinavyolenga nchi hiyo.
-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran: Adui Ametambua Lazima Aheshimu Taifa la Iran na Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Jenerali Amir Hatami amesema adui sasa ametambua kuwa hana budi kuheshimu Taifa la Iran na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu, akisisitiza kuwa msimamo na uthabiti wa wananchi wa Iran umebadili hesabu za wapinzani wao.
-
IRGC: Vikosi vya Iran Viko Tayari Kujibu Uchokozi Wowote kwa Nguvu
Naibu Kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Brigedia Jenerali Yadollah Javani, amesema silaha yenye nguvu zaidi ya Iran ni imani na itikadi ya wananchi wake, akisisitiza kuwa diplomasia na uwezo wa kijeshi vinaenda sambamba katika kulinda haki na maslahi ya taifa.
-
IRGC: Marekani Itajutia Ikiamua Kurudia Makosa Yake ya Zamani
Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Hussein Mohabbi, amesema Marekani itajutia endapo itajaribu kurudia kile alichokiita majaribio yake yaliyoshindwa dhidi ya Iran.
-
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa Apongeza Ushiriki Mkubwa wa Wananchi Baada ya Siku 100 za Mshikamano wa Kitaifa
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s), Meja Jenerali Abdollahi, amesema ushiriki mkubwa wa wananchi katika kipindi cha siku 100 zilizopita umeonyesha umoja wa kipekee wa taifa la Iran na kuwa sehemu muhimu ya nguvu za kimkakati za kuzuia maadui wa nchi hiyo.
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Hatuwezi Kuvumilia Kuendelea kwa Uhalifu Dhidi ya Lebanon
Msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran, Brigedia Jenerali Abolfazl Shekarchi, ameonya kuwa Iran haitakaa kimya mbele ya kuendelea kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon, akilaani mauaji ya raia na ukimya wa baadhi ya mataifa ya Magharibi.
-
Jenerali wa Ufaransa: Trump amenasa katika mkwamo wa kimkakati dhidi ya Iran
Jenerali wa Kifaransa Vincent Desportes amesema kuwa Donald Trump yuko katika mkwamo wa kimkakati dhidi ya Iran, akieleza kuwa licha ya Marekani kuwa na uwezo wa kijeshi wa kushambulia, bado kuna mashaka kuhusu dhamira ya kisiasa ya kuanzisha hatua hiyo.
-
Leo Katika Historia:Iran Ilishambulia Kambi ya Ain al-Asad ya Marekani kwa Makombora ya Balistiki Ikiwa Kisasi cha Kuuawa kwa Jenerali Qasim Soleimani
Ilikuwa Januari 8, 2020 pindi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilipofanya Shambulizi kubwa la Kihistoria kwa kuitwanga Kambi ya Kijeshi ya Marekani iliyoitwa "Ain al-Asad" ikiwa ni sehemu ya kulipiza kiasi baada ya Kuuawa kwa Shahidi Qassem Soleimani
-
Mkuu wa Polisi wa Iran Awaarifu Bunge Kuhusu Juhudi za Kudumisha Amani na Utulivu Nchini
Katika taarifa yake amewaeleza wabunge hatua na juhudi zinazochukuliwa na vyombo vya usalama na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha amani, utulivu na usalama vinaendelea kudumishwa nchini.
-
Muundo Mpya wa Ukuta wa Uwanja wa Palestina Tehran Wabeba Ujumbe Mkali wa Kiebrania katika Kumbukumbu ya Shahid Soleimani | Mnazidi kukaribia kutoweka
Katika kumbukumbu ya shahidi Jenerali Qasem Soleimani, jadariya jipya katika Uwanja wa Palestina, Tehran, limeibuliwa likiwa na ujumbe wa Kiebrania unaobeba onyo la kiishara kuhusu kukaribia mwisho wa zama za ubeberu na uvamizi, likisisitiza kuendelea kwa njia ya mapambano na msimamo wa upinzani.
-
-
"Tetemeko la Vitisho" – Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Atoa Onyo Kali dhidi ya “Ndoto” za Mashambulizi ya Israel!
Wachambuzi wa kijeshi wanasema lugha iliyotumiwa leo si vitisho vya kawaida, bali ni tamko rasmi kwamba Iran sasa inamiliki silaha “inayovunja mizani ya nguvu”, ambayo inaweza kufichuliwa moja kwa moja katika uwanja wa vita endapo Israel itathubutu kuchukua hatua. Ngoma za vita zinapigwa… na simba wa Iran ameonyesha meno yake!
-
Naibu Kamanda wa Vikosi vya Nchi Kavu vya Jeshi la Iran: Hatutakuwa waanzilishi wa mashambulizi kamwe
Naibu Kamanda wa Vikosi vya Nchi Kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa jeshi halitakuwa kamwe mwanzilishi wa mashambulizi, akieleza kuwa lengo la kuimarisha jeshi sio vita, bali ni kuzuia vita na kujenga uwezo wa kuzuia (deterrence).
-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC): Tukivamiwa, tutawasha moto wa Jahannam dhidi ya wavamizi
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Meja Jenerali Mohammad Pakpour, katika mazungumzo na Qasim al-A’araji, Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Iraq, amesema kuwa: “Katika vita vya siku 12, tulishambulia kwa nguvu na usahihi mkubwa na tuliharibu malengo yote yaliyolengwa.”
-
Meja Jenerali Musawi: Jeshi la Ukombozi litatoa jibu lililo juu ya fikra za waonevu (waovu)
Rais wa Makao Makuu ya Majeshi ya Ulinzi wa Iran amesema: Tunawapa uhakika wananchi wa Iran wenye heshima na ushujaa kuwa, vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu kwa kutegemea uwezo wao, ubunifu na mshangao wa kimkakati, viko tayari kukabiliana na vitisho vyovyote vya madhalimu na waonevu wa dunia kwa majibu ya wakati muafaka, makali, ya kujutia na yaliyo zaidi ya fikra zao.
-
Spika Mike Johnson Asisitiza Kuzuia Vurugu za Kisiasa Kufuatia Kifo cha Charlie Kirk
Shambulio dhidi ya Qatar lisingeweza kutokea bila kupata idhini kutoka Washington.