eneo
-
Iran: Vita vya siku 40 vimebadilisha mlinganyo wa usalama wa kikanda, vituo vya kijeshi vya kigeni vimekuwa chanzo cha kuyumbisha usalama
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema vita vya siku 40 vimebadilisha mtazamo wa nchi za eneo kuhusu mfumo wa usalama wa kikanda. Amesema uwepo wa majeshi na vituo vya kijeshi vya kigeni haukuweza kuleta usalama, bali umegeuka kuwa sababu ya kuyumbisha usalama katika eneo.
-
Mazishi ya Kamanda wa Kikosi cha Ridwan cha Hezbollah na familia yake yafanyika Beirut
Mazishi ya Ali Samir al-Haj Hasan, kamanda wa Kikosi cha Ridwan cha Hizbullah, pamoja na baadhi ya wanafamilia wake, yamefanyika katika viunga vya kusini mwa Beirut, Lebanon. Al-Haj Hasan na familia yake waliripotiwa kuuawa katika shambulio la jeshi la utawala wa Kizayuni katika eneo la Ansar, kusini mwa Lebanon.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Mlango wa Hormuz ni Sehemu Isiyotenganika ya Eneo la Ukuu wa Iran
Gholam-Hossein Mohseni Ejei amesema Mlango wa Hormuz ni sehemu ya eneo la mipaka na mamlaka ya Iran, akipuuza kauli za Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu njia hiyo ya kimataifa ya baharini.
-
Kura ya Maoni Marekani Yawapa Demokrasia Nafasi, Mvutano wa Hormuz Waongezeka huku Ripoti Zikionya Kuhusu Akiba ya Makombora ya Marekani
Kura mpya ya maoni imeonyesha kuwa wapiga kura wa Marekani sasa wanawaamini zaidi chama cha Democratic katika masuala ya uchumi kuliko Republican. Wakati huo huo, mvutano katika Mlango wa Hormuz unaendelea kuongezeka kutokana na mapendekezo mapya ya Iran, huku ripoti zikieleza kuwa jeshi la Marekani lilitumia sehemu kubwa ya makombora yake ya masafa marefu katika vita dhidi ya Iran.
-
Jenerali Rezaei: Mlango wa Hormuz hauhusiani na mfumo wa Marekani
Mwanachama wa Baraza la Utambuzi wa Maslahi ya Mfumo wa Iran, Jenerali Mohsen Rezaei, amesema Mlango wa Hormuz ni njia ya kimataifa inayotumiwa na mataifa mbalimbali na hakuna sababu kwa Marekani kuingilia suala linalohusu nchi za eneo hilo.
-
Jenerali Abdullahi: Nchi zitakazomtegemea Marekani kama ngao ya ulinzi zitaingia kwenye moto wa vita
Kamanda wa Makao Makuu ya Kati ya Khatam al-Anbiya (s.a.w), Jenerali Ali Abdullahi, ameonya nchi za eneo hilo dhidi ya kutegemea Marekani kwa ulinzi, akisema utegemezi huo unaweza kuzifanya kuwa sehemu ya migogoro na vita.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na India wazungumza kwa simu kuhusu uhusiano wa pande mbili na hali ya kikanda
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Abbas Araghchi, na mwenzake wa India, Subrahmanyam Jaishankar, wamefanya mazungumzo ya simu yaliyojikita katika kuimarisha ushirikiano wa nchi zao pamoja na kujadili maendeleo ya hivi karibuni katika eneo na duniani.
-
Mkuu wa Majeshi ya Iran: Hakuna Harakati katika Mlango wa Hormuz Bila Idhini ya Iran
Mkuu wa Majeshi ya Iran, Admiral Habibollah Sayyari, amesema vikosi vya majini vya Iran vina udhibiti kamili wa eneo la mashariki mwa Mlango wa Hormuz, Bahari ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, akisisitiza kuwa hakuna harakati zitakazoruhusiwa katika mlango huo bila idhini ya Iran.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Usimamizi Mpya wa Mlango-Bahari wa Hormuz Utawanufaisha Watu wa Kanda
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema kuwa utekelezaji wa usimamizi mpya wa Mlango-Bahari wa Hormuz kwa kuzingatia misingi ya kisheria utaleta amani, maendeleo na manufaa ya kiuchumi kwa mataifa yote ya eneo hilo.
-
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama Iran: Kuunga Mkono Marekani Kutawaletea Baadhi ya Watawala wa Eneo Hasara na Kushindwa
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Iran, Hojjatul-Islam Gholam-Hossein Mohseni Ejei, amewatahadharisha watawala wanaoitegemea Marekani na kuamini ahadi za “Shetani Mkuu”, akisema kuwa hawatapata chochote isipokuwa hasara na kushindwa.
-
Upinzani wa Iraq Waunga Mkono Mkakati wa Yemen wa Kufunga Mlango wa Bab al-Mandab
Abu Alaa al-Wala’i: “Yemen ina haki ya kufunga Mlango wa Bab al-Mandab ili dunia isikie kwamba wananchi wa Yemen hawatakufa kimya.”
-
Araghchi: Mkutano wa Rais wa Iran na Waziri Mkuu wa Iraq una umuhimu mkubwa katika mazingira ya sasa ya eneo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amesema kuwa ziara ya Waziri Mkuu wa Iraq, Ali Faleh al-Zeidi, nchini Iran ina umuhimu mkubwa kutokana na mazingira ya sasa ya eneo na inaonyesha kina cha uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
-
Mwanazuoni wa Kisunni na Imamu wa Swala ya Ijumaa Auawa Shahidi katika Shambulio la Kigaidi Kusini-Mashariki mwa Iran
Mwanazuoni wa Kisunni na Imamu wa Swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Ali Ibn Abi Talib, Molavi Mohammad Anwar Rigi, ameuawa Shahidi baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha wasiojulikana katika mji wa Mirjaveh, kusini-mashariki mwa Iran. Mamlaka za eneo hilo zimesema uchunguzi unaendelea kubaini wahusika wa shambulio hilo, huku wananchi wakitakiwa kudumisha utulivu na kutoruhusu tukio hilo kuchochea migawanyiko ya kidini.
-
Walinzi wa Mapinduzi wa Iran: Kumetokea Mlipuko Katika Meli Mbili za Mafuta Katika Mlango Bahari wa Hormuz
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wamesema meli mbili za mafuta zililipuka na kusimama baada ya kujaribu kutumia njia iliyotajwa kuwa si salama na yenye hatari katika Mlango Bahari wa Hormuz.
-
Jeshi la Iran Laangusha Ndege Isiyo na Rubani ya Adui Kusini mwa Nchi
Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuangamiza ndege isiyo na rubani ya adui aina ya “Lukas” kwa kutumia mifumo ya ulinzi wa anga ya Jeshi la Wanamaji kusini mwa nchi.
-
Makamu wa Rais wa Marekani: Mgogoro wa Iran katika Mlango wa Hormuz Hauwezi Kutatuliwa kwa Vita Pekee
Makamu wa Rais wa Marekani, J.D. Vance, amesema Marekani haitatuma wanajeshi 150,000 wa ardhini kwa lengo la kubadili utawala wa nchi nyingine, akisisitiza kuwa changamoto zinazohusisha Iran katika Mlango wa Hormuz zinahitaji suluhisho la kidiplomasia.
-
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi: Wageni Hawana Haki katika Mlango wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limesema kuwa mataifa ya kigeni hayana haki yoyote katika eneo la Iran na Mlango wa Hormuz, likionya kuwa hatua za kijeshi za Marekani zinatishia usalama wa njia hiyo muhimu ya kimataifa.
-
Jeshi la Iran: Mtu au Eneo Lolote Litakalosaidia Vikosi vya Marekani Litachukuliwa kuwa Lengo Halali
Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetoa onyo kwamba mtu, kituo au eneo lolote litakalotoa msaada kwa vikosi vya Marekani katika mashambulizi dhidi ya Iran litachukuliwa kuwa lengo halali la vikosi vya Iran.
-
Iran Yatangaza Kushambulia Malengo ya Kijeshi ya Marekani Nchini Qatar
Iran imetangaza kuwa imefanya mashambulizi dhidi ya malengo ya kijeshi ya Marekani yaliyoko nchini Qatar ikijibu mashambulizi ya Marekani Dhidi yake na katika hatua inayoashiria kuongezeka kwa mvutano wa kijeshi kati ya Tehran na Washington.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Iran Yaeleza Mkutano wa Usalama wa Marekani na Nchi za Kanda ni Maonyesho ya Kisiasa
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amesema mkutano wa kile kilichoitwa "Mazungumzo ya Usalama wa Kikanda" ulioandaliwa na Marekani nchini Bahrain ni wa maonyesho tu na unalenga kuficha sera ambazo, kwa mujibu wake, zinachochea ukosefu wa utulivu katika eneo la Asia Magharibi.
-
Maqamu ya Tall al-Zaynabiyyah katika Karbala Tukufu Yafunguliwa Rasmi Baada ya Miaka ya Ujenzi
Baada ya miaka kadhaa ya ujenzi na ukarabati, Maqam ya Tall al-Zaynabiyyah katika mji mtukufu wa Karbala imefunguliwa rasmi, na waumini wengi wamepokea kwa furaha kufunguliwa kwa eneo hili lenye umuhimu mkubwa katika historia ya tukio la Ashura.
-
Iran na Oman Zasisitiza Kutumia Fursa ya Kidiplomasia Kuimarisha Amani na Usitishaji Vita
Iran na Oman zimesisitiza umuhimu wa kutumia fursa ya sasa ya kidiplomasia kuunga mkono amani, kupunguza mvutano na kuimarisha utulivu kwa kuzingatia sheria za kimataifa na ujirani mwema.
-
Iran: Inajiandaa kwa mazungumzo muhimu, makubaliano yanahusisha utekelezaji wa vipengele 5 mara moja
Iran imetangaza kuwa inajiandaa kwa mazungumzo muhimu ya kimataifa huku ikisisitiza utekelezaji wa makubaliano ya amani, kuzuia hujuma dhidi ya mchakato huo, na kupendekeza mpango mpya wa usimamizi wa Mlango wa Hormuz ndani ya siku 60.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa Yatangaza Kushambulia Kambi za Marekani Kufuatia Uchokozi Dhidi ya Iran
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yamesema vikosi vya Jeshi la Iran na Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu vimeshambulia baadhi ya kambi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, vikieleza kuwa hatua hiyo ni jibu kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Maadhimisho Makubwa ya Eid al-Ghadir Yafanyika katika Miji Mbalimbali Duniani
Wapenzi na wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) wameadhimisha Eid al-Ghadir katika miji mbalimbali duniani kupitia mikusanyiko ya kidini, mihadhara na shughuli maalumu za kuenzi tukio hilo muhimu katika historia ya Uislamu.
-
Mohsen Rezaei: Tatizo Kuu katika Mazungumzo ni Trump Mwenyewe
Kamanda wa zamani wa Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran, Mohsen Rezaei, amesema kuwa kikwazo kikuu katika mazungumzo ni Donald Trump mwenyewe. Ameonya kuwa iwapo vita vitaanza tena, vitaweza kuenea kutoka Bahari ya Hindi hadi Bahari Nyekundu na Bahari ya Mediterania, na kuathiri usalama wa eneo kubwa la kijiografia.
-
Abdul-Malik al-Houthi: Yemen Iko Tayari kwa Hatua Yoyote ya Kuongezeka kwa Mzozo
Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Abdul-Malik al-Houthi, amesema kundi hilo liko tayari kwa hatua yoyote ya kuongezeka kwa mzozo katika Mashariki ya Kati, huku akisisitiza kuwa linaendelea kuratibu kwa karibu na washirika wake wa Muqawama kuhusu maendeleo ya Lebanon na Palestina.
-
Waumini Wahimizwa Kuzidisha Ibada na Matendo ya Kheri katika Sikukuu ya Ghadir
Sikukuu ya Ghadir, ambayo ni miongoni mwa sikukuu kubwa zaidi kwa Waislamu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari, ambapo huadhimisha ndani yake kutangazwa kwa wilayat ya Imam Ali ibn Abi Talib(as). Katika siku hii, Waumini huhimizwa kufanya amali mbalimbali za ibada na kheri kama vile kuswali, kusoma dua, kutoa sadaka na kuwalisha wengine, huku wakitumia fursa hiyo kuimarisha maarifa ya dini, kuhuisha ahadi yao katika kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) na kuimarisha mshikamano wa kijamii na kiroho.
-
Araghchi: Mashauriano kati ya Iran na Misri ni Muhimu kwa Kuimarisha Amani na Utulivu wa Kieneo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesisitiza umuhimu wa mashauriano ya pande mbili kati ya Iran na Egypt katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kukuza amani pamoja na utulivu wa kieneo, huku akitoa wito wa kutumia ipasavyo uwezo mkubwa wa nchi hizo mbili za Kiislamu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.