eneo
-
Maqamu ya Tall al-Zaynabiyyah katika Karbala Tukufu Yafunguliwa Rasmi Baada ya Miaka ya Ujenzi
Baada ya miaka kadhaa ya ujenzi na ukarabati, Maqam ya Tall al-Zaynabiyyah katika mji mtukufu wa Karbala imefunguliwa rasmi, na waumini wengi wamepokea kwa furaha kufunguliwa kwa eneo hili lenye umuhimu mkubwa katika historia ya tukio la Ashura.
-
Iran na Oman Zasisitiza Kutumia Fursa ya Kidiplomasia Kuimarisha Amani na Usitishaji Vita
Iran na Oman zimesisitiza umuhimu wa kutumia fursa ya sasa ya kidiplomasia kuunga mkono amani, kupunguza mvutano na kuimarisha utulivu kwa kuzingatia sheria za kimataifa na ujirani mwema.
-
Iran: Inajiandaa kwa mazungumzo muhimu, makubaliano yanahusisha utekelezaji wa vipengele 5 mara moja
Iran imetangaza kuwa inajiandaa kwa mazungumzo muhimu ya kimataifa huku ikisisitiza utekelezaji wa makubaliano ya amani, kuzuia hujuma dhidi ya mchakato huo, na kupendekeza mpango mpya wa usimamizi wa Mlango wa Hormuz ndani ya siku 60.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa Yatangaza Kushambulia Kambi za Marekani Kufuatia Uchokozi Dhidi ya Iran
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (s) yamesema vikosi vya Jeshi la Iran na Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu vimeshambulia baadhi ya kambi za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, vikieleza kuwa hatua hiyo ni jibu kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Maadhimisho Makubwa ya Eid al-Ghadir Yafanyika katika Miji Mbalimbali Duniani
Wapenzi na wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) wameadhimisha Eid al-Ghadir katika miji mbalimbali duniani kupitia mikusanyiko ya kidini, mihadhara na shughuli maalumu za kuenzi tukio hilo muhimu katika historia ya Uislamu.
-
Mohsen Rezaei: Tatizo Kuu katika Mazungumzo ni Trump Mwenyewe
Kamanda wa zamani wa Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran, Mohsen Rezaei, amesema kuwa kikwazo kikuu katika mazungumzo ni Donald Trump mwenyewe. Ameonya kuwa iwapo vita vitaanza tena, vitaweza kuenea kutoka Bahari ya Hindi hadi Bahari Nyekundu na Bahari ya Mediterania, na kuathiri usalama wa eneo kubwa la kijiografia.
-
Abdul-Malik al-Houthi: Yemen Iko Tayari kwa Hatua Yoyote ya Kuongezeka kwa Mzozo
Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Abdul-Malik al-Houthi, amesema kundi hilo liko tayari kwa hatua yoyote ya kuongezeka kwa mzozo katika Mashariki ya Kati, huku akisisitiza kuwa linaendelea kuratibu kwa karibu na washirika wake wa Muqawama kuhusu maendeleo ya Lebanon na Palestina.
-
Waumini Wahimizwa Kuzidisha Ibada na Matendo ya Kheri katika Sikukuu ya Ghadir
Sikukuu ya Ghadir, ambayo ni miongoni mwa sikukuu kubwa zaidi kwa Waislamu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari, ambapo huadhimisha ndani yake kutangazwa kwa wilayat ya Imam Ali ibn Abi Talib(as). Katika siku hii, Waumini huhimizwa kufanya amali mbalimbali za ibada na kheri kama vile kuswali, kusoma dua, kutoa sadaka na kuwalisha wengine, huku wakitumia fursa hiyo kuimarisha maarifa ya dini, kuhuisha ahadi yao katika kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) na kuimarisha mshikamano wa kijamii na kiroho.
-
Araghchi: Mashauriano kati ya Iran na Misri ni Muhimu kwa Kuimarisha Amani na Utulivu wa Kieneo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesisitiza umuhimu wa mashauriano ya pande mbili kati ya Iran na Egypt katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kukuza amani pamoja na utulivu wa kieneo, huku akitoa wito wa kutumia ipasavyo uwezo mkubwa wa nchi hizo mbili za Kiislamu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.
-
Iran Yalaani Vitisho vya Marekani dhidi ya Oman, Yasema Usalama wa Hormuz Unalindwa kwa Mujibu wa Sheria za Kimataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani kauli za vitisho za Marekani dhidi ya Oman akisisitiza kuwa ushirikiano wa Iran na Oman katika kulinda usalama wa usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz unafuata sheria za kimataifa na unalenga kulinda maslahi ya jamii ya kimataifa.
-
Sheikh Ahmed Al-Aameli Afanya Mkutano na Shule ya Dini ya Ali Akbar Kuhusu Tableegh Bara la India
Sheikh Ahmed Al-Aameli alikutana na uongozi na walimu wa Shule ya Dini ya Ali Akbar kujadili njia za kuimarisha mitazamo ya kisayansi katika taasisi za kidini, changamoto za Tabligh katika bara la India, na mbinu za kuendeleza juhudi za malezi ya kiroho na elimu ya dini.
-
Iraq yakataa kuruhusu matumizi ya anga lake kwa mashambulizi dhidi ya Iran
Tamko la Iraq linaonyesha kuwa Iraq inalinda mamlaka yake na haitaki kuhusishwa na migogoro ya kijeshi katika eneo hilo, ikisisitiza sera ya kudumisha usalama na utulivu wa kikanda.
-
Hashd al-Shaabi yaharibu Handaki na Maficho ya ISIS Mashariki mwa Salahuddin
Hashd Al-Shaabi ya Iraq imefanikiwa kugundua na kuharibu handaki na maficho ya ISIS Mashariki mwa Salahuddin kwa kushirikiana na jeshi la Iraq, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuzuia kurejea kwa makundi ya kigaidi katika eneo hilo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi Aongoza Ujumbe wa Mazungumzo na Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameongozana na ujumbe wake wa kidiplomasia kuelekea mjini Muscat, Oman, kwa ajili ya mazungumzo na Marekani. Mazungumzo hayo yanatazamwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujadili masuala ya nyuklia, vikwazo vya kiuchumi na usalama wa kikanda, kwa lengo la kufungua ukurasa mpya wa maelewano ya kisiasa.
-
Jibu la Kukataa la Wataalamu wa Kijeshi wa Marekani kwa Ombi Lisilo la Kawaida la Trump
Trump aliwaomba makamanda wa Marekani watengeneze shambulizi la haraka lisilogeuza vita kuwa vya muda mrefu. Wataalamu wa kijeshi wakamjibu: hakuna chaguo kama hilo linalowezekana. Wakaeleza kuwa shambulizi kubwa haliwezi kuepuka kugeuka kuwa vita ya kuchosha na ya muda mrefu.
-
Radiamali za Kimataifa kuhusu nia ya Trump kuunganisha Greenland na Marekani; Ikulu ya White House:Umuhimu wa kimkakati wa kisiwa kwa usalama wa taifa
"serikali ya Marekani kwa sasa inachunguza chaguzi mbalimbali ili kufanikisha lengo hili la kimkakati, na ikiwezekana hata “kutumia jeshi” ni miongoni mwa uwezekano unaozingatiwa na Ikulu ya White House".
-
Iran Yatuma Makundi Mawili ya Kijeshi Baharini Kulinda Meli Zake
Wachambuzi wa kimataifa wanasema kuwa hatua hii inaongeza mvutano kati ya Tehran na Washington, huku ikionyesha hatari zinazoongezeka kwa usalama wa usafirishaji wa baharini.
-
Hadhramout Yadhibitiwa na Baraza la Mpito la Kusini: Ramani Mpya ya Madaraka Mashariki mwa Yemen
Hadhramout, jimbo kubwa na lenye utajiri mkubwa zaidi nchini Yemen, limeingia rasmi kwenye udhibiti wa Baraza la Mpito la Kusini (STC) baada ya kusonga mbele kwa kasi kwa vikosi vyake. Hatua hii imeufanya mkoa huo kuwa uwanja muhimu wa kuchorwa upya kwa ramani ya madaraka mashariki mwa Yemen.
-
Daesh wabeba jukumu la shambulio dhidi ya doria ya wanamgambo wa Jolani
Daesh wametekeleza tukio la kushambulia doria inayohusiana na idara ya forodha ya Serikali ya Jolani na kuua watu wawili.
-
Iran: Kukabiliana na ugaidi kunahitaji ushirikiano wa kikanda, hasa na Afghanistan
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran alitangaza kuwa makundi ya kigaidi hayapo tu nchini Afghanistan, bali yameenea katika nchi mbalimbali za eneo hilo. Alisisitiza kuwa kukabiliana na tishio hili kunahitaji ushirikiano wa pamoja wa nchi jirani, hasa Afghanistan.
-
Utekelezaji wa programu 2,000 kwa wakati mmoja sambamba na Wiki ya Basiji katika jiji la Rasht
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (Sepah) katika eneo la kati la Rasht alisema kuwa zaidi ya programu maalumu 2,000 za Wiki ya Basiji zimepangwa kutekelezwa katika vituo vya usalama vya Basiji pamoja na maeneo ya akina kaka na dada. Alisema kuwa Basiji ni nguvu madhubuti ya nchi kwa nyanja zote.
-
Sayyid Ali Khomeini: “Kama Ubalozi wa Marekani usingelivamiwa, leo tusingekuwa na Makombora wala ishati ya nyuklia"
Akiisisitizia kauli kwamba “uvamizi wa ubalozi wa Marekani uliimarisha uhuru wa Iran,” alisema: “Kama tukio hilo lisingetokea, leo hii Jamhuri ya Kiislamu isingekuwepo, na nchi yetu isingepata teknolojia ya makombora na nishati ya nyuklia, kwani Marekani ilikuwa inapinga maendeleo haya.”
-
Ayatollah Khamenei Asifu Uwezo wa Makombora ya Iran, Asema Yameharibu Vituo Muhimu vya Utawala wa Kizayuni
Ayatollah Khamenei pia aliongeza kuwa utawala wa Kizayuni (Israel), ambao kwa muda mrefu umekuwa ukifanya vitisho na mashambulizi dhidi ya eneo hili la kikanda, sasa “umepokea funzo ambalo litabaki kwenye kumbukumbu zake,” akisisitiza kuwa taifa la Iran halitasita kujibu hatua yoyote ya uchokozi
-
Onyo la jarida la The National Interest kuhusu kuibuka kwa “Hezbollah Mpya” Katika Eneo
Jarida la Marekani “The National Interest” katika makala yake ya uchambuzi limeonesha shaka kuhusu mafanikio ya mpango wa Donald Trump wa kuleta uthabiti wa kudumu katika Ukanda wa Gaza, na limeonya kuwa mpango huo unaweza kuchangia kuibuka kwa taasisi au kundi jipya linalofanana na Hezbollah katika eneo hilo.
-
Je, Israil ni Nchi Huru au ni Jimbo linalotawaliwa na Marekani?
Kadiri ushawishi wa Marekani katika maamuzi ya Israil unavyozidi kufichuka, mijadala imeibuka ndani ya duru zisizo rasmi za utawala wa Kizayuni ikiuliza: “Je, Israil kweli ni nchi huru au ni jimbo linalotawaliwa na Marekani?” Zeev Elkin, Waziri wa Masuala ya Yerusalemu wa utawala wa Kizayuni, alijibu ukosoaji huu kwa kusema katika mahojiano ya vyombo vya habari kwamba uhusiano wa Israil na Marekani ni “ushirikiano wa kimkakati, si utegemezi.”
-
Sayyid Abdul-Malik al-Houthi: Uhalifu wa utawala wa Kizayuni unafanywa kwa msaada wa Marekani na kimya pamoja na kutochukua hatua kwa Waarabu
Mtazamo wa wazi wa Marekani inapozungumzia mabadiliko ya Mashariki ya Kati ni kubadilisha hali ya eneo hilo kwa manufaa ya adui wa Kizayuni kwa gharama ya uhuru, kujitegemea, heshima, dini na haki za mataifa ya Kiarabu na Kiislamu.
-
Netanyahu: "Tutaendelea Kuwalenga Viongozi wa Hamas"
Kiongozi wa serikali ya Kizayuni (Israel) katika mkutano wa waandishi wa habari pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, alitetea shambulio la uvamizi la taifa hilo dhidi ya Qatar lililolenga kuuwa viongozi wa Hamas, na hakukatisha nafasi ya kuonyesha kuwa shambulio kama hilo linaweza kurudiwa dhidi ya nchi nyingine za eneo.
-
“Ushirikiano wa Kutekeleza Mpango wa Marekani na Israel” / Je, “Vita kama vya Karbala” vya Hezbollah Viko Mbele
Beirut – Baadhi ya wanasiasa na wabunge wa Lebanon wamewasilisha malalamiko rasmi dhidi ya Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hizbullah, baada ya hotuba yake ya hivi karibuni aliyoituhumu serikali ya Lebanon kwa kutaka kuisalimisha nchi mikononi mwa Israel.
-
Moto Katika Msikiti wa Kihistoria wa Cordoba, Hispania
Moto uliotokea usiku katika Msikiti wa Cordoba, Hispania — ulio na historia ya zaidi ya miaka 1,000 — umezimwa kwa haraka na vikosi vya uokoaji.