hijabu

  • Umuhimu wa Hijab kwa Mwanamke: Ni kwa nini Hijab ni Wajibu kwa Mwanamke wa Kiislamu?

    Umuhimu wa Hijab kwa Mwanamke: Ni kwa nini Hijab ni Wajibu kwa Mwanamke wa Kiislamu?

    Katika zama hizi, Hijabu imelinganishwa na kutoendelea kwa jamii na inafikiriwa kuwa ni ishara ya kifungo cha wanawake. Wahubiri wengi wanafikiria kuwa ni bora kutolizungumzia jambo hili katika majlisi zao. Lakini Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Inapotokea Bid’ah na Mwanachuoni asikiseme kile akijuacho (dhidi ya Bid’ah hiyo), basi (Mwanachuoni huyo) hulaaniwa na Mwenyezi Mungu, Malaika na Wanadamu.”