Mshauri wa kijeshi wa Kiongozi Mkuu wa Iran amesema Marekani itawajibishwa iwapo kutakuwa na tishio lolote dhidi ya Iran, huku ripoti zikieleza kuwa Tehran imekataa kurejea kwenye mazungumzo ya moja kwa moja, ingawa mawasiliano kupitia wapatanishi bado yanaendelea.
Kataib Hezbollah imeonya kuwa iwapo Marekani itaanzisha vita katika eneo hilo, itakabiliwa na hasara kubwa na vita vya muda mrefu, huku pia ikiutahadharisha utawala wa Kurdistan kuepuka kushirikiana na majeshi ya kigeni.