Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Majlisi ya Shura ya Kiislamu ni kiini cha wananchi na nguzo muhimu ya sheria na utungaji wa sheria, akieleza kuwa taasisi hiyo ina jukumu la msingi katika kutekeleza matakwa ya wananchi ndani ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa Iran, hii ndiyo ustaarabu wa kale zaidi unaoendelea duniani, na daima imesimama imara mbele ya dhoruba za historia. Taifa hili, kwa roho kuu na azma isiyokoma, mara nyingi limethibitisha kwamba haliinamii mbele ya wavamizi; na leo pia limesimama kwa heshima mbele ya wanyakuzi, likitegemea nguvu ya imani na mshikamano wa kitaifa