Katika shule ya wasichana ya Shule ya Bibi Zaynab (sa) kumefanyika hafla ya kuhuisha kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s) kwa lengo la kuimarisha utamaduni wa Ashura na kuelimisha nafasi ya mwanamke katika Uislamu.
Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.