Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali kile ilichokiita “uchokozi wa kijeshi” wa Marekani dhidi ya nchi hiyo, ikisisitiza kuwa Iran haitasita kutumia haki yake ya kujilinda dhidi ya mashambulizi yoyote yanayoilenga.
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.