Katibu Mkuu wa Jumuia ya Kimataifa ya Ahlulbayt (a.s) akizungumzia hali ya sasa ya dunia:
Ameyasema kwamba jamii ya binadamu leo inakabiliwa na umasikini, ubaguzi, ukosefu wa haki, ujinga, upuuzi na ukoloni wa kihisia. Masuala haya yamezua wasiwasi mkubwa.
Aidha, tabia ya ukatili imeibuka katika baadhi ya jamii, na matukio ya uvunjaji wa haki, mauaji na vurugu yameenea.
Kwa mtazamo wa Tauhidi, kila kitu kiko mikononi mwa Mwenyezi Mungu; lakini katika maisha ya kila siku, inaonekana kana kwamba ni wanadamu wanaoamua riziki za wao kwa wao: mfanyakazi humtegemea mwajiri, mtumishi wa umma hulitegemea dola, na mtoto huwategemea wazazi. Basi ukweli wa jambo hili ni upi? Mtazamo sahihi na wa kina kuhusu suala hili ni upi?