Rais wa Brazil Lula da Silva akizungumza katika mkutano wa kimataifa mjini New York Marekani amesisitiza juu ya ulazima wa kutatuliwa kwa amani suala la Palestina na kutekelezwa kwa mapatano ya serikali mbili.
Katika taarifa ya Hizbullah na Harakati ya Amal ilisemwa: 'Enyi wafanyakazi na wazalishaji wa Lebanon, tumekuwa wavumilivu kwa muda mrefu juu ya changamoto zinazolikumba taifa letu, na sasa umefika wakati wa kuonyesha msimamo wetu wa kitaifa kwa pamoja.'
Wakaongeza: 'Tuna miadi ya kusimama kwa pamoja kama taifa, kuonyesha kupinga kwetu njia ya kujisalimisha na kutii bila masharti, na kulinda nguvu na uhuru wa Lebanon'.