Ujumbe huu unaotolewa katika mnasaba wa kumbukumbu ya Shahidi Ali Khamenei unasema hivi kuwa "Ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu ndiyo msingi wa kudumu kwa matendo mema", huku ukisisitiza kwamba athari ya kweli huzaliwa na nia safi ya kumtumikia Allah (swt).
Sheikh Athman Akbar alihimiza jamii ya Kiislamu kuiga nyayo za Imam Sajjad (a.s) kwa kuitumia dua kama silaha ya kiroho, kuimarisha subira katika majaribu, na kusimamia ukweli mbele ya dhulma ili kuendeleza ujumbe wa Karbala katika zama zote.