Lengo la si tu kufanya tamasha la filamu, bali kujenga fikra na mwelekeo wa kimataifa wa sanaa ya muqawama. Tuna ndoto ya siku ambayo tamasha hili halitafanyika tena Tehran, bali katika mji wa Quds Tukufu, pamoja na watu wa Palestina walio huru. Tamasha hili limepata pumzi yake kutoka Gaza, Lebanon, Syria, Yemen na kila uwanja wa muqawama – na litaendelea hadi kufikiwa kwa ukombozi kamili wa Quds.”