Iran imetangaza rasmi kwa mara ya kwanza kufikiwa kwa rasimu ya mwisho ya makubaliano na Marekani, huku Ijumaa ikitajwa kuwa siku ya kutiwa saini; wakati huo huo, wachambuzi wanaeleza kuwa usitishaji wa mapigano nchini Lebanon, endapo Israel itautekeleza, ni matokeo ya msimamo wa Iran wa kujumuisha suala la Lebanon katika makubaliano hayo na ustahimilivu wa Muqawama katika medani ya mapambano.
Wizara ya Ulinzi ya Israel imetiliana saini mkataba mkubwa na Kampuni ya Rafael ili kuongeza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa makombora ya kukinga ya mfumo wa Iron Dome (Gombo la Chuma).