Katika hafla iliyofanyika katika shule ya wasichana ya Kigamboni, washindi wa mashindano ya kuandika muhtasari kuhusu “Shahada ya Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)” walikabidhiwa zawadi maalum katika mwendelezo wa masomo ya Qur’an chini ya usimamizi wa Bi. Fatma Ma‘suma, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha elimu, ubunifu na ushindani wenye tija kwa wanafunzi.
Kiongozi wa chama cha Majlis Ittehad-ul-Muslimeen nchini India, akijibu mzozo ulioibuka kutokana na mabango yenye maandishi “Nampenda Muhammad” katika jimbo la Uttar Pradesh, ameishutumu serikali ya India na viongozi wa eneo hilo kwa kuweka vizuizi vya kibaguzi na vya upendeleo.