Gazeti la kila wiki la vibonzo la Charlie Hebdo la Ufaransa toleo la kesho Jumatano linatarajiwa kuchapisha kibonzo cha Mtume Muhammad katika ukurasa wake wa mbele chini ya kichwa cha habari "Yote yameshasamehewa"
Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), John Brennan, amelitetea shirika lake dhidi ya tuhuma za Baraza la Seneti kwamba wamekuwa wakitumia mateso ya kikatili kuwahoji watuhumiwa wa ugaidi.
Kamati ya seneti ya Marekani inayoshughulikia masuala ya upelelezi inatarajia kuchapisha ripoti juu ya mbinu zilizotumiwa na shirika la ujasusi CIA katika kuwahoji watuhumiwa wa ugaidi kwenye jela ya Guantanamo.