waandaaji
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) Tanzania Kuaandaa Kongamano la Kielimu Kumuenzi Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei(ra)
Kitengo cha Utafiti wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) Tawi la Dar es Salaam - Tanzania kitaandaa Kongamano la Kielimu lenye anuani "Imam Khamenei: Kutoka Jihadi hadi Ushahidi," likiwa na lengo la kuchambua kwa ufupi Maisha ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hatimaye kukuachia msikilizaji na mfuatiliaji Nafasi ya kupata mazingitio na masomo mbalimbali ya kimaisha kutoka katika kumbukumbu ya Maisha yake Matukufu, katika muktadha ule ule wa Maelekezo ya Qur'an Tukufu aliposema Mwenyezi Mungu: Hakika kuna mazingatio ndani ya visa vyao (Historia Yao) kwa watu wenye Akili"
-
Shahidi Sadr baada ya Imam na Allama alikuwa jua linalong’aa la fikra za Kiislamu katika karne ya hivi karibuni;
Tuzo ya Kitabu cha Mwaka ya Hawza inapaswa kutoka katika hali ya uzembe na kupata hadhi ya kimataifa ya marejeo
Kongamano la ishirini na saba la Kitabu cha Mwaka cha Hawza leo limegeuka kuwa jukwaa la kuenzi hadhi tukufu ya shahidi mwanazuoni, Muhammad Baqir al-Sadr, na pia kuchora upeo mpya wa tafiti na utafiti wa kielimu katika taasisi za kidini (Hawza). Tukio hilo limeangazia mchango wa kielimu na kifalsafa wa Shahidi Sadr, sambamba na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ubunifu, kina cha utafiti na upeo wa kimataifa katika kazi za kielimu za Hawza.
-
Shia Development Organization na JAI Waongoza Zoezi Kubwa la Uchangiaji Damu Bukoba
Waandaaji wa tukio hilo wamesisitiza umuhimu wa jamii kujitolea na kuwajali wananchi wasiojiweza, hususan wale waliolazwa hospitalini na wanaohitajika kuongezewa damu ili kuendelea kuishi. Wamesema misingi ya Mafundisho ya Kiislamu kupitia watukufu wa Ahlul-Bayt (a.s) inasisitiza thamani ya utu, kusaidiana na kujitoa kwa ajili ya kuimarisha ustawi wa jamii.
-
Onyesho la "Mchezo wa Kwanza" Lafanyika Katika Njia ya Arubaini
Onyesho la "Mchezo wa Kwanza" linaloongozwa na Mtayarishaji na Mkurugenzi Meisam Yusufi, litatekelezwa kama sehemu ya Maonyesho ya Tano ya Tamasha la Kimataifa la Tamthilia za Umma katika Njia ya Arubaini, linalojulikana kama "Riwaya za Wasafiri".