Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa wale wanaotumia machafuko kama njia ya kutawala mataifa mengine huishia kuwa watumwa wa machafuko hayo. Ameonya kwamba nguvu iliyoundwa kwa ajili ya kuwatawala wengine hatimaye huweza kutoka katika udhibiti wa walioiunda.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina, kupitia taarifa yake, imelaani vikali mashambulizi ya walowezi wa Kizayuni dhidi ya raia wa Kipalestina na wanaharakati wa kigeni katika msimu wa kitaifa wa uvunaji wa zeituni katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.