27 Februari 2026 - 12:40
Source: ABNA
Kiongozi wa Ansarallah: Kurekebisha Mahusiano na Israel ni Udhalimu kwa Mataifa

Kiongozi wa vuguvugu la Ansarallah la Yemen akisema kwamba kurekebisha mahusiano na utawala wa Kizayuni ni udhalimu kwa mataifa, amemtaja Israel kuwa adui dhahiri wa Uislamu.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Abna, Abdul-Malik Badruddin al-Houthi, Kiongozi wa vuguvugu la Ansarallah la Yemen, katika hotuba yake, aliyalaani mahusiano na mikataba ya baadhi ya tawala za Kiarabu na utawala wa Kizayuni na kuita kuwa ni sababu ya kuzidisha udhalimu kwa mataifa.

Aliongeza: "Ummah wa Kiislamu unakabiliwa na hatari kubwa, na kukata tamaa yoyote kutafaidisha maadui tu."

Kiongozi wa vuguvugu la Ansarallah la Yemen aliwakosoa vikali serikali na tawala zinazorekebisha mahusiano na kushirikiana na adui wa Israel na akasisitiza kwamba hatua hizi zinaongeza tu udhalimu zaidi kwa mataifa.

Akizungumzia asili ya wazi ya Israel, alisema: "Adui wa Israel haoni aibu katika kuelezea wazi nia zake za uchokozi na upanuzi wa kutawala sehemu kubwa ya jiografia ya Ummah huu."

Kiongozi wa Ansarallah akizungumzia hali ya Gaza, alisema: "Vitendo vya kihalifu vya adui wa Israel katika Ukanda wa Gaza katika kipindi cha miaka miwili iliyopita viko katika hali mbaya zaidi inayoweza kufikiriwa.

Kwa miaka miwili sasa wanafanya uhalifu huu mbaya katika Ukanda wa Gaza na bado uhalifu huu unaendelea."

Pia alikanusha madai ya Israel kuhusu umuhimu wa amani na Lebanon na akayataja matendo haya kuwa ni jaribio la "kumnyang'anya Lebanon silaha zote za nguvu."

Al-Houthi katika sehemu nyingine ya hotuba yake, alisisitiza juu ya umuhimu wa Ummah wa Kiislamu kurejea kwenye "kuamini ahadi ya kweli ya Mungu" na kutenda kwa msingi huo kwa matumaini na kumtegemea Mwenyezi Mungu na kutumia nyenzo za vitendo.

Pia akiikosoa nchi za Kiarabu ambazo zinajikita tu kutoa taarifa za kuunga mkono Palestina, aliuliza: "Je, kulaani uamuzi wa kunyakua Ukingo wa Magharibi na nchi 14 za Kiarabu kutawasaidia watu wa Palestina?"

Kiongozi wa Ansarallah aliongeza: "Utendaji wa Ummah wa Kiislamu dhidi ya Israel una athari katika kutokea mapema au kuchelewa kwa ahadi ya Mungu na ikiwa ahadi ya Mungu ya kuangamiza utawala itachelewa, gharama zitakuwa kubwa sana."

Your Comment

You are replying to: .
captcha