"Tuepuke upepo mbaya unaosambazwa kwa chuki za kidini. Sisi Waislamu hatukatazwi kuishi kwa wema na wasiokuwa Waislamu. Maisha ya watu lazima yalindwe,” alisema Mufti.
Miradi mikubwa yenye thamani ya mabilioni imetekelezwa katika mikoa mbalimbali, huku maboresho ya kiutawala na ya kimuundo yakifanikishwa, ikiwemo kuanzishwa kwa Ofisi ya Mufti, JUWAKITA na JUVIKIBA, pamoja na mabadiliko ya Katiba ya BAKWATA ili kuendana na mahitaji ya sasa.
Kwa mujibu wa Aya ya "Tathira" (Qur’an, Ahzab: 33), Ahlul-Bayt (a.s), akiwemo Imam Hussein(as), wamesafishwa (wametakaswa) na Mwenyezi Mungu dhidi ya dhambi. Hivyo, haiwezekani Imam kuwa chanzo cha fitina au kuvunja umoja.