Abu Ubaidah, msemaji wa Brigedi za Al-Qassam, ametoa wito kwa vijana wa Palestina kuongeza operesheni za mapambano dhidi ya Israel katika Ukingo wa Magharibi, huku akipongeza uthabiti wa wananchi wanaokabiliana na mashambulizi ya walowezi wa Kizayuni.
“Israel ingeweza kuwarejesha mateka wake wengi wakiwa hai miezi mingi iliyopita, lakini ilichagua kupoteza muda na kuendelea na sera ya upumbavu ya kutumia nguvu za kijeshi, jambo lililosababisha vifo vya makumi ya mateka hao mikononi mwa jeshi lake lenyewe.”