Arbaeen
-
Iran Yalaani Mashambulizi Yanayodaiwa Kufanywa na Marekani na Saudi Arabia dhidi ya Iraq na Misafara ya Mazuwwari wa Arbaeen
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na Marekani na Saudi Arabia dhidi ya maeneo rasmi nchini Iraq na misafara ya kuhudumia mazuwwari wa Arbaeen ya Imam Hussein (as), ikiyataja kuwa ni ukiukaji wa mamlaka ya Iraq na sheria za kimataifa.
-
Muqawama wa Kiislamu Iraq: Jibu kwa Marekani Halitakwepeka Baada ya Arbaeen, Yatoa Onyo kwa Serikali ya Iraq
Muqawama wa Kiislamu nchini Iraq umetangaza kuwa utatoa jibu dhidi ya kile ulichokiita mashambulizi ya Marekani baada ya kumalizika kwa ibada za Arbaeen ya Imam Hussein (as), huku ukitoa muda kwa serikali ya Iraq hadi tarehe 23 Safar kuchukua msimamo kuhusu usalama na suala la silaha za makundi ya Muqawama.
-
Tukio la Tatu la Kimataifa la “Sisi ni Wana wa Hussein (as)”
Wito kwa wanahabari, watayarishaji wa maudhui na wadau wa vyombo vya habari kushiriki katika kampeni ya kurekodi na kuhifadhi mandhari mbalimbali za Arbaeen ya Imam Hussein (as). Washiriki wanakaribishwa kutuma kazi katika nyanja za picha, video, maudhui ya Akili Bandia (AI) na podcast, zikiwemo mada maalumu kuhusu Kiongozi Shahidi katika njia ya Hussein (as) na Dunia moja katika kumbatio la Hussein (as). Kazi zinapaswa kutumwa kupitia @nahno_abna_alhussain kabla ya 22 Septemba 2026.
-
Mwakilishi wa Ayatullah Sistani:
Licha ya juhudi zote, bado haki ya kueleza na kuonesha kikamilifu ukubwa wa Arbaeen haijatimizwa
Mwakilishi mwenye mamlaka kamili wa Ayatollah Sistani nchini Iran amesema kuwa Arbaeen ni fursa kubwa sana kwa wasimamizi na wenye dhamana wa tukio hili la kimataifa, na hawapaswi kupuuzia au kughafilika na thawabu na malipo makubwa yanayopatikana kutokana nalo.
-
Ubaguzi Dhidi ya Wafuasi wa Shia Nchini Punjab: Serikali Yatumia Shinikizo na Vitisho Kukomesha Maandamano ya Arbaeen Husseini (as)
Serikali ya Punjab imewaita wamiliki wa vibali vya kufanya maombolezo, waandaaji wa vituo vya kutoa huduma za bure (maisha ya Sadaka) na wajumbe wa kamati za ulinzi, na kuwashinikiza watangaze rasmi kujitenga na matembezi ya Arbaeen kuelekea Karbala.
-
Utabiri wa Kuongezeka kwa Idadi ya Mahujaji wa Arbaeen Ikilinganishwa na Mwaka Uliopita
Haramu Takatifu ya Abbas imebashiri kuwa idadi ya mahujaji watakaoingia katika mkoa wa Karbala kwa ajili ya maadhimisho ya Arbaeen mwaka huu itaongezeka ikilinganishwa na mwaka uliopita.