Ayatollah Makarem Shirazi, mmoja wa maraja’ wa kiislamu, akisisitiza umuhimu wa kueneza habari za mafanikio ya kisayansi, alisema: “Moja ya mahitaji muhimu ya leo ni kuwafahamisha watu. Kuna shughuli nyingi zenye thamani zinafanyika, lakini taarifa zake ni chache. Vyombo vya habari, redio, televisheni na mashirika ya habari vinapaswa kusambaza maendeleo haya ili wananchi waone kiwango cha maendeleo ya teknolojia mpya katika sekta ya elimu ya dini.”
Ayatollah Makarim Shirazi amethibitisha kwamba Baraza la Uratibu wa Matangazo ya Kiislamu lina mchango mkubwa usio na mfano katika kuhifadhi mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
Ni wajibu kwa Waislamu kote duniani kuwafanya maadui hawa wajute kwa matamshi na vitendo vyao. Na ikiwa Waislamu watapata mashaka au hasara kutokana na kusimama dhidi yao, basi wao watakuwa na thawabu ya mujahid (mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu), Insha'Allah.