Ayatollah Makarem Shirazi
-
Uzinduzi wa Mfumo wa Kielelezo cha Kujadiliana na Tafsiri za Qur’ani / Ayatollah Makarem:Teknolojia Mpya Iwe Kwenye Huduma ya Qur’ani na AhlulBayt(as)
Ayatollah Makarem Shirazi, mmoja wa maraja’ wa kiislamu, akisisitiza umuhimu wa kueneza habari za mafanikio ya kisayansi, alisema: “Moja ya mahitaji muhimu ya leo ni kuwafahamisha watu. Kuna shughuli nyingi zenye thamani zinafanyika, lakini taarifa zake ni chache. Vyombo vya habari, redio, televisheni na mashirika ya habari vinapaswa kusambaza maendeleo haya ili wananchi waone kiwango cha maendeleo ya teknolojia mpya katika sekta ya elimu ya dini.”
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Baraza la Uratibu wa Matangazo Lina Nafasi Muhimu Katika Kulinda Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Ayatollah Makarim Shirazi amethibitisha kwamba Baraza la Uratibu wa Matangazo ya Kiislamu lina mchango mkubwa usio na mfano katika kuhifadhi mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Fat'wa Muhimu na Wazi ya Ayatollah Makarem Shirazi Dhidi ya Viongozi wa Kizayuni na Ubeberu
Ni wajibu kwa Waislamu kote duniani kuwafanya maadui hawa wajute kwa matamshi na vitendo vyao. Na ikiwa Waislamu watapata mashaka au hasara kutokana na kusimama dhidi yao, basi wao watakuwa na thawabu ya mujahid (mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu), Insha'Allah.
-
Ayatollah Makarem Shirazi:
Maandamano ya Siku ya Quds ni Nguvu ya Moyo kwa Mujahidina na Wanyonge wa Palestina na Lebanon
Ayatollah Makarem Shirazi, Miongoni mwa Marjii Taqlid, amewaalika Waislamu ili kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alifafanua akisema: Ni muhimu kwa viongozi na marais wa nchi za Kiislamu kuazimia na kuhakikisha azma yao ya kuacha kutojali na kupuuzia jinai za Wazayuni.