Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (AS): Kabla ya Mapinduzi, walikisema haiwezekani kuwepo kwa Mapinduzi ya Kiislamu, na wanachuoni hawakufikiri kwamba mabadiliko makubwa yangetokea nchini Iran, bali Mapinduzi ya Kiislamu yalikuwepo na yalishinda, na hayo yalikuwa ni Mapinduzi yaliyoongozwa na Kiongozi Muadhamu, na kila kitu kuhusu Mapinduzi hayo kilikuwa ni ufunuo kwa dini, kwamba hayo si chochote ila ni muujiza na kazi ya Mwenyezi Mungu.
Shahada ya Imam Ja’far al-Sadiq (a.s) haikuwa tu kumpoteza kiongozi wa kiroho, bali ilikuwa ni jaribio la kuangamiza nuru ya elimu na mwongozo wa Ahlul Bayt(a.s). Hata hivyo, athari ya mafundisho yake bado inaishi hadi leo kupitia Maktaba ya Ja’fariyya, ambayo ni msingi wa Madhehebu ya Shia Ithna ‘Ashari.