Maafisa wa Iran wamesisitiza kuwa operesheni hiyo ni sehemu ya juhudi endelevu za kupambana na magendo ya rasilimali za taifa, kulinda uchumi wa nchi, na kudumisha usalama wa majini katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
Washington Post imetahadharisha katika ripoti yake kwamba Ulaya inakabiliwa na janga la idadi ya watu; janga hili linaweza kuathiri nguvu kazi, ukuaji wa uchumi, na uthabiti wa kijamii wa bara hilo.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameweka wazi kuwa taifa la Iran halitawahi kukubali kutawaliwa na mataifa ya kigeni na litalinda uhuru wake kwa gharama yoyote.