Spika wa Bunge la Iran amesema kuwa ukiukwaji wa makubaliano ya usitishaji vita na mzingiro wa baharini unaofanywa na Marekani umechangia kuongezeka kwa mvutano katika eneo. Amesisitiza kuwa Iran itaendelea kutetea haki za wananchi wake kwa nguvu zote na kwamba vikosi vya jeshi viko tayari kukabiliana na changamoto yoyote.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema kuwa Iran haitategemea ahadi za maadui katika medani ya diplomasia, akisisitiza kuwa mafanikio hupimwa kwa matokeo halisi na kwamba umoja wa wananchi umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha nafasi ya taifa hilo katika kukabiliana na mashinikizo ya nje.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameweka wazi kuwa taifa la Iran halitawahi kukubali kutawaliwa na mataifa ya kigeni na litalinda uhuru wake kwa gharama yoyote.