Hali
-
Iran na Iraq Zakubaliana Kuimarisha Miundombinu ya Mawasiliano kwa Ajili ya Ziara ya Arubaini ya Imam Hussein (AS)
Iran na Iraq zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya mawasiliano kwa kuboresha miundombinu na kuhakikisha huduma bora, endelevu na zenye ubora wa juu kwa mamilioni ya mahujaji wa Arubaini ya Imam Hussein (AS).
-
Hali ya Majonzi Yatanda Tehran sambamba na kuanza kwa Shughuli za Kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Hali ya majonzi na huzuni kubwa imeendelea kutawala katika mji wa Tehran kuelekea shughuli za mwisho za kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei(Ra), huku umma wa Kiislamu ukiendelea kutoa heshima zake kwa Kiongozi huyu Mwema na mtetezi wa Haki za Wapalestina na Haki za wanyonge popote walipo Ulimwenguni.
-
Kamanda Matokeo Qaani: Gaza “ina tufani”, atoa onyo kali kuhusu matokeo ya kisiasa na kijeshi
Kamanda wa Kikosi cha Quds, Esmail Qaani, ametoa onyo akisema “Gaza ina tufani” na kwamba kupuuza hali halisi ya uwanja wa mapambano na kuendeshwa na maamuzi ya kisiasa kunaweza kusababisha matokeo makubwa, akirejea pia uzoefu wa Hezbollah kama mfano wa tahadhari.
-
Jeshi la Iran: Tuko tayari kutekeleza amri za Kiongozi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na kujibu ukiukaji wowote wa adui
Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuwa vikosi vyake vipo katika hali ya utayari wa juu, vikiwa “na mikono kwenye vichocheo vya silaha na masikio yakisubiri amri za Kiongozi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi,” likisisitiza kuwa litailinda Iran na maslahi yake endapo upande wa adui utakiuka makubaliano yaliyofikiwa.
-
Iran Yasitisha Mazungumzo ya Nyuklia na Marekani Kufuatia Mashambulizi ya Israel Lebanon
Iran imesitisha safari ya ujumbe wake kwenda Geneva kwa ajili ya duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia na Marekani, ikieleza kuwa kuendelea kwa mashambulizi ya Israel kusini mwa Lebanon kumekiuka mazingira ya kusitisha mapigano. Kufuatia msimamo huo, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, naye ameripotiwa kusitisha safari yake, huku hali hiyo ikiweka mashaka juu ya kuanza kwa mazungumzo yaliyokuwa yanatarajiwa kuwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Waislamu wa Argentina Wakati wa Ramadhani: Hali ya Kipekee na Ushiriki wa Kipekee wa Kiimani
Mwezi wa Ramadhani nchini Argentina unaenda sambamba na siku za kufunga zinazodumu chini ya saa 9, jambo linalotoa hali tofauti ya kiroho na kimvuto cha kiimani. Hali hii inarahisisha waislamu kushiriki kwa uhuru zaidi katika ibada zao za Ramadhani na kuimarisha mshikamano wa kijamii na kifamilia.
-
Baghdad yafuatilia kuongezeka kwa uwepo wa ISIS
Wasiwasi wa kiusalama nchini Iraq kuhusu shughuli za ISIS mpakani na Syria umeongezeka, licha ya hatua kali za kiusalama, huku kukiwa na maonyo ya kiintelijensia na ongezeko la tahadhari.
-
Mkutano wa Kwanza wa Mielekeo ya Kiislamu Umefanyika nchini Ureno kwa Lengo la Kukuza Mazungumzo ya Kidiini +Picha
Kundi la wasomi wa Kiislamu na Kikristo limekutana katika mji mkuu wa Ureno, Lisbon, kujadili nafasi ya Ushi’a, mazungumzo ya dini tofauti, pamoja na fursa za pamoja za dini katika kufanikisha amani ya dunia.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain:
Kujiondoa kwenye njia ya Muqawama (Mapambano ya kupinga dhulma) ni sawa na fedheha na udhalili
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain alisisitiza kuwa kuacha njia ya Muqawama (mapambano dhidi ya wavamizi na dhulma) hakuzai chochote isipokuwa fedheha, udhalilishaji na utumwa.