Wasiwasi wa kiusalama nchini Iraq kuhusu shughuli za ISIS mpakani na Syria umeongezeka, licha ya hatua kali za kiusalama, huku kukiwa na maonyo ya kiintelijensia na ongezeko la tahadhari.
Kundi la wasomi wa Kiislamu na Kikristo limekutana katika mji mkuu wa Ureno, Lisbon, kujadili nafasi ya Ushi’a, mazungumzo ya dini tofauti, pamoja na fursa za pamoja za dini katika kufanikisha amani ya dunia.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain alisisitiza kuwa kuacha njia ya Muqawama (mapambano dhidi ya wavamizi na dhulma) hakuzai chochote isipokuwa fedheha, udhalilishaji na utumwa.