Huruma
-
Vipi tunaweza kujiona ni wenye thamani?
“Heshima ya Nafsi” ni mojawapo ya misingi muhimu ya maisha ambayo ina nafasi maalumu katika mafundisho ya Kiislamu. Dhana hii, tofauti na kiburi, inategemea kutambua thamani halisi ya mwanadamu na ni njia ya kuinua utu wa kiroho na kijamii. Kwa maneno mengine, heshima ya nafsi inamaanisha kuwa mtu anaona thamani yake kwa mujibu wa viwango vya kweli vya kiroho na maadili, akiepuka hisia za kujiboresha kwa kulinganishwa na wengine au kujivunia bila sababu. Hii huimarisha tabia za busara, huruma, na uthabiti wa kiroho, na pia husaidia mtu kuishi kwa heshima na wengine katika jamii.
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum: Swaumu ya Ramadhan si adhabu, bali ni Tiba ya Kiroho na Kimwili
Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum anafafanua kuwa swaumu ya mwezi mtukufu wa Ramadhan si adhabu, bali ni ibada iliyojaa huruma ya Mwenyezi Mungu. Kufunga kunalenga kutuponya kiroho na kimwili, kuimarisha nafsi, na kutufundisha subira, kama ambavyo Daktari (Tabibu) humlazimisha mgonjwa kunywa dawa chungu, lakini sio kwa lengo la kumuadhibu, bali ili apone. Swaumu ni fursa ya kujenga uhusiano thabiti baina ya Mja na Mola wake (swt) na kupata manufaa mapana katika maisha yetu.
-
Mkuu wa Mahusiano ya Kigeni wa Hizbullah ya Lebanon: Umoja wa Kiislamu ni dhamana ya ushindi wa Umma dhidi ya utawala wa Kizayuni
Mkuu wa Mahusiano ya Kigeni na Mjumbe wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi umoja wa Kiislamu na kufuata mafundisho ya Mtume Mtukufu Muhammad (s.a.w.w) kuhusu huruma na uongofu, akieleza juu ya juhudi endelevu za maadui katika kuharibu sura ya Uislamu.
-
Arubaini ya Imam Hussein (a.s):
Taasisi za Kijamii Nchini Tanzania: BEF na Nyota Foundation Zandaa Tukio la Uchangiaji Damu kwa Upendo na Huruma ya Kibinadamu
Tukio hili limeonesha mshikamano wa kijamii na mshikikano wa kiimani kwa kuenzi mfano wa kujitolea na ubinadamu wa Imam Hussein (a.s), na limekuwa ni ishara muhimu ya mshikamano wa Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla katika kusaidia wenzao wenye uhitaji wa Damu Mahospitalini.
-
Hospitali ya Ebrahim Hajji Charitable Healthcare Yatangaza Upimaji Bure wa Saratani Kwa Wananchi - Dkt. Molloo Aeleza Mpango Kabambe
“Upimaji wa Saratani tofauti kama ya shingo ya kizazi, matiti, na tezi dume kwa wanaume utafanyika bure kabisa. Wengine watapata matibabu hapo hapo na wale wanaohitaji huduma maalum zaidi watapewa rufaa,” alisema Dkt. Molloo.
-
Picha ya Kusikitisha Gaza; Mama Aliyejeruhiwa na Mtoto Akiwa na Kifuko cha Damu Mkononi!
Picha hii ya kusikitisha kutoka Gaza inaonyesha mama mmoja aliyejeruhiwa na mtoto wake ambaye amebeba kifuko cha damu mkononi. Hii ni picha ya maumivu na mateso makubwa yanayowakumba watu wasio na hatia, hasa watoto na familia zao katika maeneo ya vita.
-
Madrasat Hazrat Zainab (SA) - Kigamboni | Imam Hussein (A.S) ni Mlango wa Rehema Pana ya Mwenyezi Mungu
Imam Hussein (A.S) alikuwa ni mfano wa rehema ya Mwenyezi Mungu duniani. Mapambano na msimamo wake ni darasa kwa Umma. Kwa hiyo: 1_Waislamu waitikie wito wa Imam Hussein (A.S). 2_Waonyeshe huruma kwa wengine. 3_Watubu na wafanye toba kwa kupitia Ahlulbayt ili kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu.