Kibinadamu
-
Reza Pahlavi mara nyingine tena akitaka shambulio la kijeshi dhidi ya Iran!
Reza Pahlavi amekuwa akipigia debe uingiliaji wa kijeshi dhidi ya Iran, akidai kuzingatia madai ya "uingiliaji wa kibinadamu," huku akiungwa mkono na kushiriki moja kwa moja katika matukio ya kigaidi na mashambulio ya kijeshi, jambo linaloonyesha uhusiano wake na mikakati ya kigaidi na vitisho vya kijeshi.
-
Kwa mwaka wa tatu mfululizo; Sudan yaongoza orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani
Sudan kwa mwaka wa tatu mfululizo imeorodheshwa juu kabisa katika orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani.Nchi nyingine zilizoorodheshwa katika ripoti hiyo ni pamoja na: Myanmar, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mali, Burkina Faso, Lebanon, Afghanistan, Cameroon, Chad, Colombia, Niger, Nigeria, Somalia, Syria, Ukraine na Yemen.
-
Mwakilishi wa Kiongozi wa Kidini katika Taasisi ya Mashujaa:
"Tutaendeleza vita dhidi ya ubeberu hadi bendera ya haki itakapoinuliwa juu"
Sheikh Hujjatul-Islam wal-Muslimin Musavi Muqaddam, Mwakilishi wa Kiongozi wa Kidini (Waliyyul-Faqih) katika Taasisi ya Mashujaa na Masuala ya Wapiganaji wa Kiislamu, amesema kuwa: "Tuna malengo makubwa, na kwa ajili ya kuyafikia tutaendelea kujitahidi na kusimama imara. Tutaendeleza vita dhidi ya ubeberu hadi pale bendera ya haki itakapoinuliwa na thamani za kibinadamu zitakapohifadhiwa."
-
Italia na Hispania Zimetuma Manowari za Kivita kwa ajili ya Kulinda Msafara wa Meli za Sumuud
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.