Kibinadamu
-
Mwakilishi wa Kiongozi wa Kidini katika Taasisi ya Mashujaa:
"Tutaendeleza vita dhidi ya ubeberu hadi bendera ya haki itakapoinuliwa juu"
Sheikh Hujjatul-Islam wal-Muslimin Musavi Muqaddam, Mwakilishi wa Kiongozi wa Kidini (Waliyyul-Faqih) katika Taasisi ya Mashujaa na Masuala ya Wapiganaji wa Kiislamu, amesema kuwa: "Tuna malengo makubwa, na kwa ajili ya kuyafikia tutaendelea kujitahidi na kusimama imara. Tutaendeleza vita dhidi ya ubeberu hadi pale bendera ya haki itakapoinuliwa na thamani za kibinadamu zitakapohifadhiwa."
-
Italia na Hispania Zimetuma Manowari za Kivita kwa ajili ya Kulinda Msafara wa Meli za Sumuud
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.
-
Kuuawa Shahidi na Kujeruhiwa kwa Wapalestina 373 ndani ya masaa 24
Wizara ya Afya ya Gaza imetangaza kuuawa Shahidi na kujeruhiwa Wapalestina 373 katika muda wa saa 24 zilizopita na kuongezeka kwa idadi ya Mashahidi wa mauaji ya kimbari na kufikia zaidi ya watu 50,600.