Mchambuzi wa zamani wa CIA Larry Johnson amesema mashambulizi dhidi ya Iran wakati mazungumzo yakiendelea yanaashiria juhudi za kuhujumu mchakato wa kidiplomasia, akionya kuwa huenda eneo hilo likashuhudia duru mpya ya mvutano katika siku zijazo.
Kwa upande wake, Balozi Lentz alieleza kuwa ushirikiano wa Tanzania na Marekani umejengwa katika misingi ya ustawi wa pamoja, si utegemezi wa misaada, na kupongeza juhudi za Tanzania chini ya falsafa ya 4R na Dira ya Maendeleo ya 2050. Takribani makampuni 400 ya Marekani yanafanya kazi nchini, jambo linaloonesha kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji.