Hezbollah imesema imefanya operesheni 22 za kijeshi kwa kutumia makombora, ndege zisizo na rubani na mizinga dhidi ya vikosi vya Israel kusini mwa Lebanon, ikidai kuharibu magari ya kijeshi, kulenga vituo vya kijeshi na kulazimisha ndege ya Israel ya aina ya Hermes 450 kuondoka katika anga la Lebanon.
Katika mwendelezo wa operesheni za kijeshi za utawala wa Israel ndani ya ardhi ya Syria, doria kadhaa za jeshi la Israel zimeingia katika vijiji vya mkoa wa Quneitra na kufanya ukaguzi wa nyumba za wananchi.