Mahakama Kuu ya Shirikisho ya Iraq imetangaza rasmi kumalizika kwa muhula wa tano wa Bunge la nchi hiyo, na kuitaja serikali ya sasa kuwa ni “serikali ya kusimamia mambo ya kila siku”, yenye mamlaka tu katika kushughulikia masuala ya kawaida na yasiyoweza kuahirishwa.
Ismail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, amelaani na kulikemea tamko la Kundi la G7 kuhusu suala la nyuklia la Iran, akilitaja kuwa ni la kinafiki na kupotosha ukweli.