Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum amewahimiza Waumini wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuhudhuria kwa wingi, akisisitiza kuwa mwaka huu Maulid itakuwa na vionjo vya pekee, ikiwa ni kumbukumbu ya kumsifu na kufuata nyayo za Mtume Muhammad (s.a.w).
Sherehe hiyo ya Mazazi ya Mtume wa Ummah (saww), imeonesha mshikamano, mapenzi ya dhati, na hamasa kubwa ya waislamu katika kuenzi maisha na mafundisho ya Mtume Muhammad (s.a.w.w). Idadi kubwa ya washiriki katika hafla hii imekuwa ishara tosha ya mafanikio makubwa ya tukio hilo takatifu, na ushahidi wa mapenzi ya kweli kwa Mtume wa Mwisho