Masheikh
-
Ujumbe wa Wanazuoni wa Palestina Wawasili Iran Kutoa Heshima kwa Mwili Msafi wa Shahidi aliyeishi kwa kutetea Quds na Watu wa Palestina
Ujumbe wa masheikh na wanazuoni kutoka Palestina umewasili Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa ajili ya kutoa heshima na kuonesha mshikamano wao kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Iran Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra); huku ukisisitiza nafasi ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu katika kuunga mkono Quds Tukufu na haki za wananchi wa Palestina.
-
Maulid Kubwa Masjid Majmuuat - Temeke Mwisho Kufanyika Ijumaa Oktoba 17, 2025
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum amewahimiza Waumini wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuhudhuria kwa wingi, akisisitiza kuwa mwaka huu Maulid itakuwa na vionjo vya pekee, ikiwa ni kumbukumbu ya kumsifu na kufuata nyayo za Mtume Muhammad (s.a.w).
-
Maulid ya Kitaifa 2025 Yang'ara Tanga | Rais wa Jamiat al-Mustafa (s) - Tanzania Sh.Dr. Ali Taqavi Ajumuika na Umma Kuadhimisha Maulid ya Mtume (saww)
Sherehe hiyo ya Mazazi ya Mtume wa Ummah (saww), imeonesha mshikamano, mapenzi ya dhati, na hamasa kubwa ya waislamu katika kuenzi maisha na mafundisho ya Mtume Muhammad (s.a.w.w). Idadi kubwa ya washiriki katika hafla hii imekuwa ishara tosha ya mafanikio makubwa ya tukio hilo takatifu, na ushahidi wa mapenzi ya kweli kwa Mtume wa Mwisho