Mataifa
-
Iraq Yaandaa Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)
Marasimu ya kihistoria ya mazishi ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Hussein Khamenei, pamoja na mashahidi wa familia yake, yanafanyika leo nchini Iraq kwa ushiriki wa maelfu ya waombolezaji.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso: Iran imekuwa mfano wa kipekee wa heshima na uhuru
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso, Karamoko Jean Marie Traoré, amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa mfano wa kipekee wa heshima, uhuru na ustahimilivu, akipongeza msimamo thabiti wa wananchi wa Iran katika kukabiliana na vitisho na mashinikizo visivyo halali.
-
Araghchi aishukuru Thailand kwa mshikamano wake na Iran kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameishukuru Thailand kwa jumbe zake za pole na mshikamano kwa serikali na wananchi wa Iran, huku akieleza kuthamini ushiriki wa mwakilishi wa nchi hiyo katika shughuli za kumuaga Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Khamenei (r.a.).
-
Sheikh Naim Qassem: Iran ni Alama ya Heshima na Nguzo ya Muqawama Dhidi ya Israel
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amesema katika barua yake kwa Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, kwamba Iran imeonyesha kwa vitendo uungaji mkono wake kwa haki, muqawama na waliodhulumiwa. Ameeleza kuwa mchango wa Iran umeimarisha uwezo wa Lebanon kujitetea na kuitaja Iran kuwa "alama ya heshima na utukufu" katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni.
-
Baghaei: Nguvu Waliyoiumba kwa Ajili ya Kuwatawala Wengine Imetoka Mikononi Mwao
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa wale wanaotumia machafuko kama njia ya kutawala mataifa mengine huishia kuwa watumwa wa machafuko hayo. Ameonya kwamba nguvu iliyoundwa kwa ajili ya kuwatawala wengine hatimaye huweza kutoka katika udhibiti wa walioiunda.
-
Mwanajeshi wa Zamani wa Jeshi la Marekani Atembelea Haram ya Bibi Fatima Ma'suma (a.s) Mjini Qum
Mwanajeshi wa zamani wa Jeshi la Wanamaji la Marekani, Nicholas Ken O'Keefe, ametembelea Haram Tukufu ya Bibi Fatima Ma'suma (a.s) mjini Qum nchini Iran wakati wa ziara yake nchini humo.
-
Kampeni ya Kimataifa Yazinduliwa Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kiongozi Shahidi Kupitia Qur’ani, Dua na Ziara za Maeneo Matakatifu
Shirika la International Union of One Ummah limezindua kampeni ya kimataifa inayohamasisha usomaji wa Qur’ani Tukufu, dua, tawafu na ziara za maeneo matakatifu kwa lengo la kuenzi kumbukumbu ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, huku wanazuoni wa Iraq wakitoa wito kwa mahujaji kushiriki katika ibada maalumu za kumkumbuka.
-
Timu ya Wanawake ya Volleyball ya Iran Yatwaa Ubingwa wa CAVA kwa Mara ya Pili Mfululizo
Timu ya taifa ya wanawake ya volleyball ya Iran imeendelea kuonesha ubabe wake katika ukanda wa Asia ya Kati baada ya kutwaa ubingwa wa Mashindano ya CAVA 2026 kwa kuifunga Kazakhstan mabao 3-1 katika mchezo wa fainali uliofanyika mjini Kathmandu, Nepal.
-
Rais wa Cuba: Mataifa ya Amerika ya Kusini Lazima Yaungane
Rais wa Cuba ametoa wito kwa mataifa ya Amerika ya Kusini kuimarisha umoja wao kufuatia operesheni ya kijeshi ya Marekani iliyosababisha kukamatwa kwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, akitaja hatua hiyo kuwa ni “shambulio la kinyama” dhidi ya taifa huru.
-
Imani ya Mahdawi: Vipi Iliwafanya Waislamu wa Kishia Kusimama Imara Katika Mitihani Mikubwa ya Ulimwengu wa Kiislamu?
Madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s), likiwa limejengwa juu ya itikadi ya kumwamini Imam Mahdi (a.t.f.s) aliyeahidiwa kwa mataifa yote, linabeba mafundisho yenye utajiri mkubwa kuhusu uadilifu na uokovu. Mafundisho haya yamewafanya Waislamu wa Kishia kubaki imara, thabiti na wenye heshima katika mitihani na misukosuko mikubwa ya ulimwengu wa Kiislamu.
-
Nafasi ya Marājiʿ wa Kishia katika Kulinda Umoja wa Ardhi na Utambulisho wa Kitaifa- Sehemu ya 2 | Marāji ni, Walinzi wa Uhuru wa Nchi za Kiislamu
Mfano mashuhuri ni Ayatullah al-Uzma Sayyid Muhammad Hasan Shirazi, ambaye alitoa Fat'wa maarufu ya kupiga marufuku tumbaku mwaka 1891 huko Iran, hatua iliyozuia njama za kikoloni za Waingereza na kuwa alama ya mapambano ya Kiislamu dhidi ya ukoloni. Vivyo hivyo, Ayatullah Kashif al-Ghita, Ayatullah Muhsin al-Hakim, na Imam Khomeini (r.a) walikuwa mstari wa mbele katika kuhimiza mapambano ya kulinda utu, uhuru, na heshima ya mataifa ya Kiislamu.
-
China Yaonesha Nguvu za Kijeshi Katika Gwaride Huku Rais wa China Xi Akisimama Pamoja na Rais Putin na Rais Kim +Picha
China iliandaa gwaride kubwa la kijeshi kuonesha uwezo wake wa kivita, huku Rais Xi Jinping akisalimiana na kusimama pamoja na Rais Vladimir Putin wa Urusi na Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un. Hafla hiyo iliangazia umoja wa kisiasa kati ya mataifa hayo na kuonesha silaha mpya na teknolojia ya kisasa ya kijeshi mbele ya maelfu ya watazamaji na viongozi wa kimataifa.