Mbalimbali
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Araghchi aishukuru Thailand kwa mshikamano wake na Iran kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameishukuru Thailand kwa jumbe zake za pole na mshikamano kwa serikali na wananchi wa Iran, huku akieleza kuthamini ushiriki wa mwakilishi wa nchi hiyo katika shughuli za kumuaga Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Khamenei (r.a.).
-
Qalibaf Akutana na Spika wa Bunge la Iraq Pembeni ya Shughuli za Maombolezo Tehran
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amekutana na Spika wa Bunge la Iraq, Heibat Al-Halbousi, aliyefika Tehran akiwa na ujumbe wa wabunge kushiriki katika shughuli za maombolezo na kuaga kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Diplomasi wa Iraq Athibitisha Ushiriki wa Raia Wake na Kujadili Mradi wa Reli Kati ya Iran–Iraq
Balozi Mkuu wa Iraq katika Mji wa Kermanshah, Saadoun Al-Saadi, amesema makundi mbalimbali ya wananchi wa Iraq yako tayari kushiriki katika shughuli za kijamii na pia amejadili na viongozi wa Iran kuhusu mradi wa reli unaounganisha Kermanshah na Baghdad kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi.
-
Rais Pezeshkian: Umoja wa Kitaifa Ndiyo Mtaji Mkubwa Zaidi wa Iran Katika Kipindi Hiki
Rais Masoud Pezeshkian amesema mshikamano wa kitaifa ndio msingi wa maendeleo ya Iran, akisisitiza matumizi ya uwezo wa wataalamu na kujibu mahitaji ya wananchi ili kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
-
Mkurugenzi Mkuu wa IRNA: Sehemu ya Migongano ya Dunia Leo Inaendeshwa Kupitia Vita vya Maarifa na Simulizi
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRNA), Hussein Jaberi Ansari, amesema kuwa vyombo vya habari vimekuwa nguzo muhimu ya nguvu, ushawishi na hata usalama wa taifa, huku akisisitiza kuwa sehemu kubwa ya migongano ya dunia inaendeshwa kupitia vita vya kiakili na mapambano ya simulizi.
-
Mwanajeshi wa Zamani wa Jeshi la Marekani Atembelea Haram ya Bibi Fatima Ma'suma (a.s) Mjini Qum
Mwanajeshi wa zamani wa Jeshi la Wanamaji la Marekani, Nicholas Ken O'Keefe, ametembelea Haram Tukufu ya Bibi Fatima Ma'suma (a.s) mjini Qum nchini Iran wakati wa ziara yake nchini humo.
-
Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel anatarajiwa katika kikao chake na Rais wa Marekani
Kuwasilisha chaguo mbalimbali za mashambulizi mapya yanayoweza kufanywa na Israel dhidi ya Iran, pamoja na kujadiliana kuhusu hali tofauti za kijeshi na athari zake kwa usalama wa kikanda.
-
Upinzani wa Iraq: Hatutokabidhi silaha zetu, na tunasimama imara dhidi ya shinikizo la Marekani
Haider Al-Khayoun, mhadhiri wa siasa za kimataifa, alibainisha kuwa vitisho vya Marekani na Israel dhidi ya Iraq si vipya, lakini kwa sasa vimekuwa tata zaidi kutokana na ukosefu wa serikali thabiti yenye uwezo wa kuchukua maamuzi ya kimkakati. Alisisitiza kuwa Iraq ni sehemu ya mlinganyo mpana wa kikanda unaojumuisha Iran, Syria, Lebanon na Gaza, na kwamba kuongezeka kwa mvutano katika maeneo hayo kuna athari za moja kwa moja kwa Baghdad.
-
Jeshi la Lebanon liliwaruhusu waandishi wa habari kuingia katika vituo vya Hizbullah;
JKituo cha kihistoria cha Muqawama ambacho ukweli wake umejulikana baada ya kusitishwa kwa mapigano
Bonde la Zabqin, kutokana na muundo wake maalum wa kijiografia na umbali wa takribani kilomita 10 kutoka mpaka wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu, linachukuliwa kuwa mojawapo ya ngome kuu za Muqawama (Upinzani). Ni ngome ambayo vizazi mbalimbali vya wapiganaji wa Kipalestina na Wenyeji wa Lebanon wamekuwa wakikuwapo humo kwa miaka mingi.
-
Marekani imeweka vikwazo dhidi ya watu 100 na taasisi mbalimbali kwa sababu ya kununua mafuta kutoka Iran
Serikali ya Donald Trump imeweka vikwazo vipya dhidi ya takriban watu 100, makampuni, na meli. Watu na taasisi hizi wanashutumiwa kushiriki katika ununua na usafirishaji wa mafuta na bidhaa za petrochemical za Iran.