Mfupi
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) Tanzania Kuaandaa Kongamano la Kielimu Kumuenzi Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei(ra)
Kitengo cha Utafiti wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) Tawi la Dar es Salaam - Tanzania kitaandaa Kongamano la Kielimu lenye anuani "Imam Khamenei: Kutoka Jihadi hadi Ushahidi," likiwa na lengo la kuchambua kwa ufupi Maisha ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hatimaye kukuachia msikilizaji na mfuatiliaji Nafasi ya kupata mazingitio na masomo mbalimbali ya kimaisha kutoka katika kumbukumbu ya Maisha yake Matukufu, katika muktadha ule ule wa Maelekezo ya Qur'an Tukufu aliposema Mwenyezi Mungu: Hakika kuna mazingatio ndani ya visa vyao (Historia Yao) kwa watu wenye Akili"
-
Kundi la “Hanzala” Latuma Onyo Kali kwa Jeshi la Wanamaji la Marekani, Latishia Majibu Makali
Kundi la mtandao linalojiita “Hanzala” limetoa onyo kali kwa wanamaji wa Jeshi la Wanamaji la Marekani, likiwataka kuwasiliana na familia zao, likidai kuwa makombora yako tayari na likitahadharisha kujibu kwa nguvu iwapo kutatokea uchokozi dhidi ya Iran.
-
Trump: Lebanon Si Sharti Katika Makubaliano ya Muda Mfupi Kati ya Marekani na Iran
Rais Donald Trump amesema kuwa Marekani haitoi sharti la Lebanon kujumuishwa katika makubaliano ya muda mfupi na Iran, huku akisisitiza kuwa kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Tehran kutategemea kufikiwa kwa makubaliano ya amani kwanza.
-
Abbas Araghchi: Makubaliano yako karibu iwapo diplomasia itapewa kipaumbele
Abbas Araghchi amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani yako ndani ya mfukoni iwapo diplomasia itapewa kipaumbele, akisisitiza kuwa Iran haitafuti silaha za nyuklia lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya teknolojia ya amani ya nyuklia.
-
Maneno Mafupi, Yenye Maana Pana:
Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha: "Kuwa na mzigo mwepesi ili mfike (kwenye safari yenu)!"
تَخَفَّفُوا تَلْحَقُوا، فَإِنَّمَا يُنْتَظَرُ بِأَوَّلِكُمْ آخِرُكُمْ "Punguzeni mizigo ili mfike (kwenye malengo ya safari yenu), kwa maana waliotangulia wanawasubiri mlio nyuma." Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha – Mtazamo wa Akhera katika Jitihada za Binadamu: Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha inaangazia maisha ya binadamu kwa mtazamo wa akhera, na inaeleza kwamba: Binadamu anapaswa kuwa mwepesi wa mizigo (wa kidunia), ili aweze kwa urahisi kutoka duniani na kuelekea kwenye maisha ya akhera. Hili linaonyesha kuwa jitihada za binadamu si kwa ajili ya dunia pekee, bali kwa ajili ya ukamilifu wa kiutu (kamilifu) na maisha ya milele.