Amesema kuwa uongo mwingi kuhusu Iran unatolewa na taasisi zinazopingwa na msimamo wa Iran wa kusimama dhidi ya Marekani na Israel. Hata hivyo, baada ya vita vya siku kumi na mbili, wanafikra wengi duniani wamekiri wazi kwamba Iran ndilo taifa pekee lililosimama dhidi ya dhulma kwa njia ya kivitendo, si kwa maneno tu.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameweka wazi kuwa taifa la Iran halitawahi kukubali kutawaliwa na mataifa ya kigeni na litalinda uhuru wake kwa gharama yoyote.