Muumini
-
"Mtu kama mimi hawezi kumpa baia mtu kama yeye" – Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alipofafanua somo Kubwa la Muharram
Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alisema kuwa somo kubwa zaidi la Mwezi wa Muharram ni kujitolea kwa Imam Hussein (AS) kwa ajili ya kuilinda dini ya Uislamu, akisisitiza kuwa kila Muumini anapaswa kuwa tayari kujitoa kwa kila alicho nacho pale utetezi wa Uislamu unapohitajika.
-
Mtume Muhammad (saww)anasema: "Upendo kwa Fatima unafaa (unamnufaisha muumini) katika sehemu mia - hususan wakati wa Mauti, kaburini na katika Sirati"
Mtume (saww) anatuambia: Ikiwa unampenda Fatima (a.s) kwa moyo wa kweli, basi upendo huo utakuwa mwanga, kinga, na msaada wako katika hatua ngumu zaidi za Akhera.
-
Katika Kikao cha "Nafasi ya Wanawake wa Vyombo vya Habari katika Muqawama (Mapambano - Upinzani) ilibainika:
Kutoka kwa Zainab al-Kubra(s) hadi leo; Karbala ni Chuo cha Habari cha Mwanamke Muumini /Wanawake Waislamu wako mstari wa mbele katika vita vya Habari
Misingi Mitatu ya Wajibu wa Mwanamke Mwislamu katika Ulimwengu wa Habari Kueneza uelewa: Mwanamke Mwislamu anapaswa kuwa sauti ya ukweli, afichue upotoshaji wa vyombo vya habari vya upande wa uongo, na atangaze mateso ya waliodhulumiwa duniani – kuanzia Palestina hadi kila sehemu inayokandamiza utu. Kutetea utambulisho: Vyombo vya habari vya kisasa vinajaribu kumvua mwanamke heshima yake na kumgeuza bidhaa ya matangazo. Mwanamke Mwislamu lazima athibitishe kuwa uhalisia na usasa vinaweza kuishi pamoja, na kwamba heshima hupimwa kwa utiifu wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu, si kwa uchi au mvuto wa sura. Kulea kizazi cha waandishi wa kweli: Wajibu wa mwanamke hauishii katika kushiriki binafsi katika vyombo vya habari; anatakiwa kulea kizazi kinachotambua nguvu ya neno na dhamana ya uandishi wa ukweli.