Baadhi ya wanaharakati na wafuasi wa Palestina nchini Afrika Kusini wanashona vipande vya kitambaa vyenye rangi za bendera ya Palestina, kuunda kazi ya ishara ya kumbukumbu kwa watoto waliopoteza maisha katika vita vya Ghaza. Kazi hii itafunguliwa rasmi mnamo tarehe 29 Novemba, Siku ya Kimataifa ya Umoja na Palestina.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameweka wazi kuwa taifa la Iran halitawahi kukubali kutawaliwa na mataifa ya kigeni na litalinda uhuru wake kwa gharama yoyote.