Swala ya jamaa ni mkusanyiko wa kifahari zaidi, bora zaidi, safi zaidi, na wa kiroho zaidi duniani. Kwa sababu hiyo, ina fadhila na thawabu nyingi. Kwa kila hatua anayopiga mtu kuelekea swala ya jamaa, huandikiwa thawabu na wema. Na iwapo idadi ya waswaliji itazidi watu kumi, basi hakuna ajuaye kiwango cha thawabu isipokuwa Mwenyezi Mungu tu.
Sala ya Jamaa ni Kinga dhidi ya Shetani. Na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) alisema: فإنَّما يأكلُ الذئبُ منَ الغنمِ القاصيةَ / “Hakika mbwa mwitu humla Kondoo aliyejitenga.”