Beirut – Baadhi ya wanasiasa na wabunge wa Lebanon wamewasilisha malalamiko rasmi dhidi ya Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hizbullah, baada ya hotuba yake ya hivi karibuni aliyoituhumu serikali ya Lebanon kwa kutaka kuisalimisha nchi mikononi mwa Israel.
Uchunguzi mpya wa maoni nchini Lebanon umeonyesha kuwa Wana-Lebanon wengi—bila kujali dini au dhehebu—wanapinga kuondolewa silaha za vikosi vya mapambano bila kuwepo mkakati mbadala wa ulinzi.