Maandamano ya 22 Bahman kwa maadhimisho ya miaka 47 ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yameripotiwa kwa upana na vyombo vya habari vya Kiarabu. Mitandao kama Al-Mayadeen, Al-Manar na Al-Masirah pamoja na magazeti ya Ra’i Al-Youm na Al-Arabi Al-Jadeed yaliripoti ushiriki mkubwa wa wananchi katika Tehran na zaidi ya miji 1200, yakitaja hotuba ya rais kuhusu kuimarisha uhusiano na majirani na kuoneshwa kwa mafanikio ya kijeshi kama alama ya upya wa ahadi kwa malengo ya Mapinduzi.