تَخَفَّفُوا تَلْحَقُوا، فَإِنَّمَا يُنْتَظَرُ بِأَوَّلِكُمْ آخِرُكُمْ "Punguzeni mizigo ili mfike (kwenye malengo ya safari yenu), kwa maana waliotangulia wanawasubiri mlio nyuma." Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha – Mtazamo wa Akhera katika Jitihada za Binadamu:
Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha inaangazia maisha ya binadamu kwa mtazamo wa akhera, na inaeleza kwamba:
Binadamu anapaswa kuwa mwepesi wa mizigo (wa kidunia), ili aweze kwa urahisi kutoka duniani na kuelekea kwenye maisha ya akhera.
Hili linaonyesha kuwa jitihada za binadamu si kwa ajili ya dunia pekee, bali kwa ajili ya ukamilifu wa kiutu (kamilifu) na maisha ya milele.
Mja asikose wala asikate tamaa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani, bali akithirishe kwa wingi kuomba sana maghfira na msamaha kwa Mwenyezi Mungu, kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, na anasamehe dhambi za aina yoyote ile (ispokuwa dhambi ya kumshirikisha).