dhambi

  • Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Atoa Nasaha za Eid al-Adha na Hijja: Ibada Ifanywe kwa Ikhlasi na Si Kujionesha Mitandaoni

    Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Atoa Nasaha za Eid al-Adha na Hijja: Ibada Ifanywe kwa Ikhlasi na Si Kujionesha Mitandaoni

    Sheikh Profesa Alhad Mussa Salum amesisitiza umuhimu wa uelewa sahihi wa ibada za Eid al-Adha na Hijja. Ameeleza kuwa kondoo ni mnyama bora zaidi kwa kuchinjwa katika Eid al-Adha endapo anapatikana, na hata nyama yake ni bora zaidi Bali Kondoo Ndiye asili ya ibada hiyo. Kuhusu Hijja, amebainisha kuwa ni ibada ya kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu kupitia Nabii Ibrahim (as), na huleta utakaso wa dhambi kwa mja. Ameonya baadhi ya mahujaji kukosa maandalizi ya kiroho na kurejea katika dhambi baada ya Hijja. Ameikosoa tabia ya kutumia ibada ya Hijja kwa kujionesha mitandaoni kupitia Picha za “selfie”, akisisitiza kuwa ibada ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee. Amemalizia kwa kusisitiza msingi wa ikhlasi na kuepuka riyaa katika ibada zote.

  • Utawala wa Saudi umemnyonga kijana mmoja wa Shi’a kutoka Qatif

    Utawala wa Saudi umemnyonga kijana mmoja wa Shi’a kutoka Qatif

    Wapinzani wa Saudi wameeleza kuwa Mohammed Al-Ammar hakuwa mtenda dhambi wala mwanamgambo; bali alikuwa kijana aliyeota uhuru, heshima, na haki za kijamii. Lakini utawala ambao haukubali mazungumzo, unapandisha mti wa kifo mbele ya sauti ya uhuru, na hukata vichwa dhidi ya yale yanayodaiwa kwa amani.

  • Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha: "Kuwa na mzigo mwepesi ili mfike (kwenye safari yenu)!"

    Maneno Mafupi, Yenye Maana Pana:

    Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha: "Kuwa na mzigo mwepesi ili mfike (kwenye safari yenu)!"

    تَخَفَّفُوا تَلْحَقُوا، فَإِنَّمَا يُنْتَظَرُ بِأَوَّلِكُمْ آخِرُكُمْ "Punguzeni mizigo ili mfike (kwenye malengo ya safari yenu), kwa maana waliotangulia wanawasubiri mlio nyuma." Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha – Mtazamo wa Akhera katika Jitihada za Binadamu: Hotuba ya 21 ya Nahjul Balagha inaangazia maisha ya binadamu kwa mtazamo wa akhera, na inaeleza kwamba: Binadamu anapaswa kuwa mwepesi wa mizigo (wa kidunia), ili aweze kwa urahisi kutoka duniani na kuelekea kwenye maisha ya akhera. Hili linaonyesha kuwa jitihada za binadamu si kwa ajili ya dunia pekee, bali kwa ajili ya ukamilifu wa kiutu (kamilifu) na maisha ya milele.