ghadir

  • Majibu kwa Shubuhati Zinazohusu Wilayat na Uimamu, na Siri Iliyofichika katika Tukio la Ghadir

    Majibu kwa Shubuhati Zinazohusu Wilayat na Uimamu, na Siri Iliyofichika katika Tukio la Ghadir

    «وَلَوْ شِئْتُ أَنْ أُسَمِّیَ الْقَائِلِينَ بِذَلِكَ بِأَسْمَائِهِمْ لَسَمَّيْتُ ... وَلَكِنِّي وَاللَّهِ فِي أُمُورِهِمْ قَدْ تَكَرَّمْتُ» "Na kama ningetaka kuwataja wale waliotoa maneno hayo kwa majina yao, basi ningewataja. Lakini kwa hakika, kwa jina la Mwenyezi Mungu, nimewatendea kwa ukarimu na staha katika mambo yao." Kauli hii inaonyesha kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwajua wanafiki mmoja baada ya mwingine na alikuwa na uwezo wa kuwataja waziwazi. Hata hivyo, kutokana na hekima, ukarimu na maslahi ya Umma wa Kiislamu, hakufanya hivyo. Je, jambo hili lina maana kwamba Mtume (s.a.w.w.) alipuuza wajibu wake? Hapana. Kusudi la utume halikuwa tu kufichua watu, bali lilikuwa kuongoza jamii, kuwapa nafasi ya kutubia na kurejea katika haki, pamoja na kulinda umoja wa Waislamu dhidi ya fitina kubwa zaidi. Kama Mtume (s.a.w.w.) angewataja wanafiki wote hadharani, huenda baadhi yao wangetangaza uasi wao dhidi ya Uislamu, jambo ambalo lingeweza kusababisha migawanyiko mikubwa na hata vita vya ndani katika jamii changa ya Kiislamu. Kwa hiyo, kunyamaza kwake kuhusu majina yao hakukuwa udhaifu wala kuacha wajibu, bali ilikuwa ni sehemu ya hekima ya uongozi wa Mtume katika kuhifadhi maslahi makubwa ya dini na jamii.

  • “Utetezi Mtakatifu (Kujihami Kutakatifu - Sacred Defence) ni chuo cha malezi na hazina ya kitamaduni”

    Naibu wa Ofisi ya Tablighi ya Hawza ya Qom amesema kuwa:

    “Utetezi Mtakatifu (Kujihami Kutakatifu - Sacred Defence) ni chuo cha malezi na hazina ya kitamaduni”

    Hujjatul-Islam Rousta Azad amesema: Kongamano la “Muballighina Mujahid” likiambatana na kumbukumbu ya kuwatunukia mfano bora wa jihadi na tabligh, litafanyika siku ya Jumatano, tarehe 9 Mehr, kuanzia saa 3 asubuhi, kwa kuhudhuriwa na kundi muhimu la makamanda na mashahidi hai wa Vita vya Utetezi Mtakatifu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Ghadir, Ofisi ya Tablighi ya Kiislamu.

  • Utabiri wa Mazuwwari 8 Milioni Katika Siku za Mwisho za Mwezi wa Safar

    Utabiri wa Mazuwwari 8 Milioni Katika Siku za Mwisho za Mwezi wa Safar

    Naibu wa Kitengo cha Utamaduni, Jamii na Hija wa Mkoa wa Khorasan Razavi, Hojjatoleslam Ali Asgari, amesema kuwa idadi ya mazuwwari katika siku za mwisho za mwezi Safar imeongezeka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka uliopita. Kwa kuzingatia likizo zinazokaribia, inatarajiwa kuwa idadi ya mazuwwari itafikia takriban milioni 8.

  • Ghadir inachukuliwa kuwa ni harakati ya kuunganisha Uislamu | Kama Kusingekuwa na Ghadir, Uislamu Halisi ungeamizwa na Bani Umaiyya na Bani Abbas

    Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt(AS):

    Ghadir inachukuliwa kuwa ni harakati ya kuunganisha Uislamu | Kama Kusingekuwa na Ghadir, Uislamu Halisi ungeamizwa na Bani Umaiyya na Bani Abbas

    Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (AS): Kabla ya Mapinduzi, walikisema haiwezekani kuwepo kwa Mapinduzi ya Kiislamu, na wanachuoni hawakufikiri kwamba mabadiliko makubwa yangetokea nchini Iran, bali Mapinduzi ya Kiislamu yalikuwepo na yalishinda, na hayo yalikuwa ni Mapinduzi yaliyoongozwa na Kiongozi Muadhamu, na kila kitu kuhusu Mapinduzi hayo kilikuwa ni ufunuo kwa dini, kwamba hayo si chochote ila ni muujiza na kazi ya Mwenyezi Mungu.