Kiongozi Muadhamu wa Jamhuri ya kiislamu ya Iran katika hafla ya sherehe za Eid Ghadir amesema kuwa Marekani na washirika wake hawapo kupambana na Magaidi wa Daesh bali kuchochea tofauti kati ya waislamu.
Hijja hii ilihudhuruwa na maswahaba wengi sana, inasemekana kuwa idadi yao ilikuwa takriban watu laki moja na ishirini na nne elifu (124000), watu hawa katika siku ya jummamosi tarehe 24 mwezi wa Dhilqa’adah wakiwa sanjari na mtume Muhammad s.a.w waliongozana kuelekea katika mji mtukufu wa Makka kwa ajili ya kutekeleza Ibada ya hijja.