ghadir
-
Naibu wa Ofisi ya Tablighi ya Hawza ya Qom amesema kuwa:
“Utetezi Mtakatifu (Kujihami Kutakatifu - Sacred Defence) ni chuo cha malezi na hazina ya kitamaduni”
Hujjatul-Islam Rousta Azad amesema: Kongamano la “Muballighina Mujahid” likiambatana na kumbukumbu ya kuwatunukia mfano bora wa jihadi na tabligh, litafanyika siku ya Jumatano, tarehe 9 Mehr, kuanzia saa 3 asubuhi, kwa kuhudhuriwa na kundi muhimu la makamanda na mashahidi hai wa Vita vya Utetezi Mtakatifu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Ghadir, Ofisi ya Tablighi ya Kiislamu.
-
Utabiri wa Mazuwwari 8 Milioni Katika Siku za Mwisho za Mwezi wa Safar
Naibu wa Kitengo cha Utamaduni, Jamii na Hija wa Mkoa wa Khorasan Razavi, Hojjatoleslam Ali Asgari, amesema kuwa idadi ya mazuwwari katika siku za mwisho za mwezi Safar imeongezeka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka uliopita. Kwa kuzingatia likizo zinazokaribia, inatarajiwa kuwa idadi ya mazuwwari itafikia takriban milioni 8.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt(AS):
Ghadir inachukuliwa kuwa ni harakati ya kuunganisha Uislamu | Kama Kusingekuwa na Ghadir, Uislamu Halisi ungeamizwa na Bani Umaiyya na Bani Abbas
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (AS): Kabla ya Mapinduzi, walikisema haiwezekani kuwepo kwa Mapinduzi ya Kiislamu, na wanachuoni hawakufikiri kwamba mabadiliko makubwa yangetokea nchini Iran, bali Mapinduzi ya Kiislamu yalikuwepo na yalishinda, na hayo yalikuwa ni Mapinduzi yaliyoongozwa na Kiongozi Muadhamu, na kila kitu kuhusu Mapinduzi hayo kilikuwa ni ufunuo kwa dini, kwamba hayo si chochote ila ni muujiza na kazi ya Mwenyezi Mungu.