ibrahim Traore
-
Burkina Faso Yakanusha Taarifa za Machafuko; Serikali Yatetea Muswada wa Kudhibiti Maeneo ya Ibada
Serikali ya Burkina Faso imetetea hatua ya kumkamata mwanazuoni wa Kiislamu Dk. Mohamed Kindou kufuatia hotuba yake kuhusu muswada wa maeneo ya ibada, huku ikisisitiza kuwa hakuna uasi dhidi ya Rais Ibrahim Traoré na kwamba wananchi bado wanaunga mkono uongozi wake.
-
Burkina Faso, Mali na Niger Zazindua Operesheni ya Pamoja ya Kijeshi Dhidi ya Makundi ya Kijihadi
Kiongozi wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré, ametangaza kuanza kwa hatua mpya za kijeshi katika eneo la Sahel baada ya nchi yake, kwa kushirikiana na Mali na Niger, kuzindua operesheni ya pamoja inayolenga kukabiliana na makundi ya kijihadi yanayohusishwa na Al-Qaeda na ISIS. Hatua hiyo inakuja katika muktadha wa kuimarishwa kwa muungano wa kijeshi wa nchi hizo tatu, huku zikisisitiza mshikamano wa kiusalama na mwelekeo mpya wa ushirikiano wa kikanda kufuatia kujiondoa kwao katika ECOWAS na kuvunja ushirikiano wa awali na Ufaransa na Marekani.
-
Burkina Faso: Daktari Aliyemkosoa Rais Traoré Atumwa Vitani kupambana na Magaidi Baada ya kupata Mafunzo ya Kijeshi - Kisa Kinachozua Mjadala Mpana
Rais Ibrahim Traoré, akizungumza katika mahojiano ya televisheni ya kitaifa, alithibitisha tukio hilo na kusema kwa maneno makali: “Kama kuna daktari, mwalimu, au mfanyabiashara anayehisi anajua zaidi kuhusu vita kuliko wanajeshi wetu, basi ni bora naye achangie kwa vitendo - aende vitani.”