Kiongozi wa kiitikadi wa Mashia alisema kuwa: ‘Msikiti usio na vijana hauwezi kustawi, na uwepo wa vijana katika misikiti ni wa thamani sana.’ Alisisitiza: ‘Ninashukuru na kupongeza jitihada za Vikundi vya Utamaduni na Sanaa vya Misikiti katika shughuli za Qur’an na uhai wa misikiti, na nina matumaini uwepo wa vijana katika misikiti utakuwa mkubwa zaidi.
Katika Muktadha wa Wiki ya Utetezi Mtakatifu (Sacred Defence), tafsiri ya Kiarabu ya kitabu “Hekalu ya Chini ya Ardhi” kilichoandikwa na Ma‘sumeh Mirabutalebi, ambacho kimepambwa na (maoni ya kupongeza) ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu (Ayatollah Khamenei), kimechapishwa na Dar Tamkin nchini Iraq.