Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani kauli za vitisho za Marekani dhidi ya Oman akisisitiza kuwa ushirikiano wa Iran na Oman katika kulinda usalama wa usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz unafuata sheria za kimataifa na unalenga kulinda maslahi ya jamii ya kimataifa.
Urusi imependekeza mpango wa makubaliano kati ya Iran na Marekani. Kampuni ya Urusi Rosatom isimamie urutubishaji wa urani nchini Iran kwa matumizi ya kiraia. Iran ibaki na haki ya kurutubisha urani kwa kiwango cha karibu 3.6%. Iran itoe dhamana ya kutotumia makombora yake kwa mashambulizi ya mapema dhidi ya Marekani au Israel.
Lengo ni kufikia makubaliano yanayokubalika kwa pande zote.